< Ufunuo 13 >

1 Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari. Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru.
And I stood on the sea sand. And I saw a beast rise out of the sea, hauing seuen heads, and ten hornes, and vpon his hornes were ten crownes, and vpon his heads the name of blasphemie.
2 Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa.
And the beast which I sawe, was like a Leopard, and his feete like a beares, and his mouth as the mouth of a lion: and the dragon gaue him his power and his throne, and great authoritie.
3 Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama.
And I sawe one of his heads as it were wounded to death, but his deadly wound was healed, and all the world wondred and folowed the beast.
4 Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”
And they worshipped the dragon which gaue power vnto the beast, and they worshipped the beast, saying, Who is like vnto the beast! who is able to warre with him!
5 Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
And there was giuen vnto him a mouth, that spake great things and blasphemies, and power was giuen vnto him, to doe two and fourtie moneths.
6 Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni.
And he opened his mouth vnto blasphemie against God, to blaspheme his Name, and his tabernacle, and them that dwell in heauen.
7 Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa.
And it was giuen vnto him to make warre with the Saints, and to ouercome them, and power was giuen him ouer euery kinred, and tongue, and nation.
8 Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
Therefore all that dwell vpon the earth, shall worship him, whose names are not written in the booke of life of that Lambe, which was slaine from the beginning of the world.
9 Yeye aliye na sikio na asikie.
If any man haue an eare, let him heare.
10 Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka, atachukuliwa mateka. Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.
If any leade into captiuitie, hee shall go into captiuitie: if any kill with a sword, he must be killed by a sword: here is the patience and the faith of the Saints.
11 Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka.
And I beheld another beast comming vp out of the earth, which had two hornes like the Lambe, but he spake like the dragon.
12 Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.
And he did all that the first beast could doe before him, and he caused the earth, and them which dwell therein, to worship the first beast, whose deadly wound was healed.
13 Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi.
And he did great wonders, so that hee made fire to come downe from heauen on the earth, in the sight of men,
14 Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi.
And deceiued them that dwell on the earth by the signes, which were permitted to him to doe in the sight of the beast, saying to them that dwell on the earth, that they should make the image of the beast, which had the wound of a sword, and did liue.
15 Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa.
And it was permitted to him to giue a spirit vnto the image of the beast, so that the image of the beast should speake, and should cause that as many as would not worship the image of the beast, should be killed.
16 Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso,
And he made all, both small and great, rich and poore, free and bond, to receiue a marke in their right hand or in their foreheads,
17 ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.
And that no man might buy or sell, saue hee that had the marke, or the name of the beast, or the number of his name.
18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.
Here is wisdome. Let him that hath wit, count the number of the beast: for it is the number of a man, and his number is sixe hundreth threescore and sixe.

< Ufunuo 13 >