< Ufunuo 13 >
1 Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari. Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru.
Now I was standing on the seashore, and I saw a Beast of prey coming up out of the sea, having seven heads and ten horns, and on his horns ten diadems and on his heads blasphemous names.
2 Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa.
The beast that I saw was similar to a leopard, his feet were like those of a bear, and his mouth was like a lion's mouth. And the dragon gave him his power and his throne and great authority.
3 Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama.
And one of his heads was as if it had been mortally wounded, but his fatal wound was healed. And the whole earth marveled after the Beast.
4 Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”
And they did obeisance to the dragon who had given the authority to the Beast, and they did obeisance to the Beast saying, “Who is like the Beast, and who is able to make war with him?”
5 Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
And he was given a mouth speaking great things, that is, blasphemy; and he was given authority to make war forty-two months.
6 Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni.
So he opened that mouth of his in blasphemy against God, to blaspheme His name and His tabernacle, those who dwell in Heaven.
7 Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa.
And it was given to him to make war with the saints and to conquer them. And authority was given him over every tribe and language and ethnic nation.
8 Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
All who dwell on the earth will do obeisance to him, whose names have not been written in the Book of Life of the Lamb slaughtered from the foundation of the world.
9 Yeye aliye na sikio na asikie.
If anyone has an ear, let him hear.
10 Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka, atachukuliwa mateka. Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.
If anyone has captivity, he goes away. If anyone kills with the sword, with the sword he must be killed. Here is the endurance and the faith of the saints.
11 Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka.
Now I saw another beast of prey coming up out of the land, and he had two horns like a lamb and spoke like a dragon.
12 Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.
And he exercises all the authority of the first Beast in his presence; and he started to cause the earth and those who dwell in it to worship the first Beast, whose mortal wound was healed.
13 Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi.
And he performs great signs, including that fire should come down from heaven upon the earth before the people.
14 Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi.
And he deceives my own people, those dwelling on the earth, by the signs that it was given to him to perform before the Beast, telling those who dwell on the earth to make an image to the Beast who had the sword wound and lived.
15 Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa.
And it was granted to him to give breath to the image of the Beast, so that the image of the Beast should actually speak, and should cause as many as would not worship the image of the Beast to be killed.
16 Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso,
And he causes everyone—both small and great, both rich and poor, both free and slave—to receive marks on their right hand or on their foreheads,
17 ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.
so that no one would be able to buy or sell who does not have the mark, the name of the Beast or the number of his name.
18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.
Here is wisdom: let the one who has understanding evaluate the number of the Beast, for it is the number of man—his number is 666.