< Ufunuo 11 >
1 Ndipo nikapewa mwanzi uliokuwa kama ufito wa kupimia, nikaambiwa, “Nenda ukapime hekalu la Mungu pamoja na madhabahu, nawe uwahesabu wale waabuduo humo.
And there was given to me a reed like to a rod, [[and the messenger stood, ]] saying, “Rise, and measure the temple of God, and the altar, and those worshiping in it;
2 Lakini usiupime ua wa nje wa Hekalu, uache, kwa sababu ua huo wamepewa watu wa Mataifa. Hao wataukanyagakanyaga mji mtakatifu kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
and leave out the court that is outside the temple, and you may not measure it, because it was given to the nations, and they will tread down the holy city forty-two months;
3 Nami nitawapa mashahidi wangu wawili uwezo, nao watoe unabii kwa muda wa siku 1,260, wakiwa wamevaa nguo za gunia.”
and I will give to My two witnesses, and they will prophesy one thousand, two hundred, sixty days, clothed with sackcloth”;
4 Hawa ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili vya taa visimamavyo mbele za Bwana Mungu wa dunia yote.
these are the two olive [trees], and the two lampstands that stand before the God of the earth;
5 Kama mtu yeyote akitaka kuwadhuru, moto hutoka vinywani mwao na kuwateketeza adui zao. Hivi ndivyo impasavyo kufa mtu yeyote atakayetaka kuwadhuru.
and if anyone may will to injure them, fire proceeds out of their mouth, and devours their enemies, and if anyone may will to injure them, thus it is required of him to be killed.
6 Watu hawa wanao uwezo wa kufunga anga ili mvua isinyeshe wakati wote watakapokuwa wanatoa unabii wao. Nao watakuwa na uwezo wa kuyabadili maji kuwa damu na kuipiga dunia kwa kila aina ya mapigo mara kwa mara kama watakavyo.
These have authority to shut the sky, that rain may not rain in the days of their prophecy, and they have authority over the waters to turn them to blood, and to strike the land with every plague, as often as they may will.
7 Basi watakapokuwa wamemaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika lile Shimo atapigana nao vita, atawashinda na kuwaua. (Abyssos )
And when they may finish their testimony, the beast that is coming up out of the abyss will make war with them, and overcome them, and kill them, (Abyssos )
8 Maiti zao zitabaki katika barabara ya mji mkubwa, ambao kwa fumbo unaitwa Sodoma na Misri, ambapo pia Bwana wao alisulubiwa.
and their body [is] on the street of the great city that is called spiritually Sodom and Egypt, where also their Lord was crucified,
9 Kwa muda wa siku tatu na nusu, watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa wataziangalia hizo maiti zao na hawataruhusu wazikwe.
and they gaze—[those] of the peoples, and tribes, and tongues, and nations—on their dead bodies three and a half days, and they will not allow their dead bodies to be put into tombs,
10 Watu waishio duniani watazitazama kwa furaha maiti za hao manabii wawili na kushangilia kwa kupeana zawadi kwa sababu hao manabii waliwatesa watu waishio duniani.
and those dwelling on the earth will rejoice over them, and will make merry, and they will send gifts to one another, because these—the two prophets—tormented those dwelling on the earth.
11 Lakini baada ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu ikawaingia, nao wakasimama kwa miguu yao na wote waliowaona wakaingiwa na hofu kuu.
And after the three and a half days, [the] Spirit of life from God entered into them, and they stood on their feet, and great fear fell on those beholding them,
12 Kisha wale manabii wawili wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, “Njooni huku juu!” Nao wakapaa mbinguni katika wingu, wakati adui zao wakiwa wanawatazama.
and they heard a great voice out of Heaven saying to them, “Come up here”; and they went up to Heaven in the cloud, and their enemies beheld them;
13 Saa iyo hiyo, kukatokea tetemeko kubwa la nchi na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka. Watu elfu saba wakauawa katika tetemeko hilo, nao walionusurika wakaogopa sana, wakamtukuza Mungu wa mbinguni.
and in that hour a great earthquake came, and the tenth of the city fell, and seven thousand names of men were killed in the earthquake, and the rest became frightened, and they gave glory to the God of Heaven.
14 Ole ya pili imekwisha kupita, tazama ole ya tatu inakuja upesi.
The second woe went forth, behold, the third woe comes quickly.
15 Yule malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake, pakawa na sauti kubwa mbinguni iliyosema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala milele na milele.” (aiōn )
And the seventh messenger sounded the trumpet, and there came great voices in Heaven, saying, “The kingdoms of the world became [those] of our Lord and of His Christ, and He will reign through the ages of the ages!” (aiōn )
16 Nao wale wazee ishirini na wanne, waliokuwa wameketi mbele za Mungu, kwenye viti vyao vya enzi, wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu,
And the twenty-four elders, who are sitting on their thrones before God, fell on their faces and worshiped God,
17 wakisema: “Tunakushukuru, Bwana Mungu Mwenyezi, uliyeko na uliyekuwako, kwa kuwa umetwaa uweza wako mkuu na ukaanza kutawala.
saying, “We give thanks to You, O LORD God, the Almighty, who is, and who was, and who is coming, because You have taken Your great power and reigned;
18 Mataifa walikasirika nao wakati wa ghadhabu yako umewadia. Wakati umewadia wa kuwahukumu waliokufa na kuwapa thawabu watumishi wako manabii na watakatifu wako pamoja na wale wote wanaoliheshimu Jina lako, wakubwa kwa wadogo: na kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.”
and the nations were angry, and Your anger came, and the time of the dead to be judged, and to give the reward to Your servants, to the prophets, and to the holy ones, and to those fearing Your Name, to the small and to the great, and to destroy those who are destroying the earth.”
19 Ndipo hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana humo ndani. Kukatokea mianga ya umeme wa radi, ngurumo, sauti za radi, tetemeko la nchi na mvua kubwa ya mawe.
And the temple of God was opened in Heaven, and the Ark of His Covenant was seen in His temple, and there came lightnings, and voices, and thunders, and an earthquake, and great hail.