< Ufunuo 11 >

1 Ndipo nikapewa mwanzi uliokuwa kama ufito wa kupimia, nikaambiwa, “Nenda ukapime hekalu la Mungu pamoja na madhabahu, nawe uwahesabu wale waabuduo humo.
I was given a reed like a measuring rod. And the angel stood saying: “Rise and measure the temple of God and the altar, and those who worship there.
2 Lakini usiupime ua wa nje wa Hekalu, uache, kwa sababu ua huo wamepewa watu wa Mataifa. Hao wataukanyagakanyaga mji mtakatifu kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
But leave out the outer court of the temple and do not measure it, because it has been given to the nations; and they will trample the holy city for forty-two months.
3 Nami nitawapa mashahidi wangu wawili uwezo, nao watoe unabii kwa muda wa siku 1,260, wakiwa wamevaa nguo za gunia.”
And I will give authority to my two witnesses, and they will prophesy one thousand two hundred and sixty days, clothed in sackcloth.”
4 Hawa ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili vya taa visimamavyo mbele za Bwana Mungu wa dunia yote.
These are the two olive trees, even the two lampstands that stand before the Lord of the earth.
5 Kama mtu yeyote akitaka kuwadhuru, moto hutoka vinywani mwao na kuwateketeza adui zao. Hivi ndivyo impasavyo kufa mtu yeyote atakayetaka kuwadhuru.
And if anyone wants to harm them fire comes out of their mouths and consumes their enemies. So if anyone wants to harm them he must be killed in this way.
6 Watu hawa wanao uwezo wa kufunga anga ili mvua isinyeshe wakati wote watakapokuwa wanatoa unabii wao. Nao watakuwa na uwezo wa kuyabadili maji kuwa damu na kuipiga dunia kwa kila aina ya mapigo mara kwa mara kama watakavyo.
They have authority to shut up the sky so that no rain falls during the days of their prophecy; and they have authority over the waters to turn them into blood, and to strike the earth with every plague, as often as they wish.
7 Basi watakapokuwa wamemaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika lile Shimo atapigana nao vita, atawashinda na kuwaua. (Abyssos g12)
When they finish their witness, the Beast of prey that comes up out of the Abyss will make war with them, overcome them and kill them (Abyssos g12)
8 Maiti zao zitabaki katika barabara ya mji mkubwa, ambao kwa fumbo unaitwa Sodoma na Misri, ambapo pia Bwana wao alisulubiwa.
—and leave their corpses in the street of the great city! (which is called Sodom and Egypt, spiritually speaking), even where their Lord was crucified.
9 Kwa muda wa siku tatu na nusu, watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa wataziangalia hizo maiti zao na hawataruhusu wazikwe.
And those from the peoples, tribes, languages and ethnic nations look at their corpses three and a half days, and will not allow their corpses to be buried.
10 Watu waishio duniani watazitazama kwa furaha maiti za hao manabii wawili na kushangilia kwa kupeana zawadi kwa sababu hao manabii waliwatesa watu waishio duniani.
And those who dwell on the earth rejoice over them, and they will enjoy themselves and send gifts to one another, because these two prophets tormented those who dwell on the earth.
11 Lakini baada ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu ikawaingia, nao wakasimama kwa miguu yao na wote waliowaona wakaingiwa na hofu kuu.
And after three and a half days a breath of life from God entered them and they stood on their feet, and a great fear fell on those who were watching them.
12 Kisha wale manabii wawili wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, “Njooni huku juu!” Nao wakapaa mbinguni katika wingu, wakati adui zao wakiwa wanawatazama.
And I heard a loud voice from the heaven saying to them, “Come up here!” And they went up to heaven in a cloud, and their enemies watched them.
13 Saa iyo hiyo, kukatokea tetemeko kubwa la nchi na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka. Watu elfu saba wakauawa katika tetemeko hilo, nao walionusurika wakaogopa sana, wakamtukuza Mungu wa mbinguni.
And in that day there was a severe earthquake and a tenth of the city fell, and seven thousand individuals were killed in the earthquake. And the rest became fearful and gave glory to the God of heaven.)
14 Ole ya pili imekwisha kupita, tazama ole ya tatu inakuja upesi.
The second woe is past. Look out, here comes the third woe!
15 Yule malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake, pakawa na sauti kubwa mbinguni iliyosema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala milele na milele.” (aiōn g165)
So the seventh angel trumpeted, and there were loud voices in heaven saying: “The kingdom of the world has become the kingdom of our Lord and of His Christ, and He shall reign forever and ever!” (aiōn g165)
16 Nao wale wazee ishirini na wanne, waliokuwa wameketi mbele za Mungu, kwenye viti vyao vya enzi, wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu,
And the twenty-four elders, who sit on their thrones in God's presence, fell on their faces and worshiped God
17 wakisema: “Tunakushukuru, Bwana Mungu Mwenyezi, uliyeko na uliyekuwako, kwa kuwa umetwaa uweza wako mkuu na ukaanza kutawala.
saying: “We thank You, O Lord God Almighty, He who is and who was and who is coming, because You have taken up your great power and begun to reign.
18 Mataifa walikasirika nao wakati wa ghadhabu yako umewadia. Wakati umewadia wa kuwahukumu waliokufa na kuwapa thawabu watumishi wako manabii na watakatifu wako pamoja na wale wote wanaoliheshimu Jina lako, wakubwa kwa wadogo: na kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.”
The nations were angry and your wrath came, even the time for the dead to be judged and to give the reward to Your slaves the prophets, and to the saints and those who fear your name, small and great, and to destroy those who have corrupted the earth.”
19 Ndipo hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana humo ndani. Kukatokea mianga ya umeme wa radi, ngurumo, sauti za radi, tetemeko la nchi na mvua kubwa ya mawe.
And the temple of God in heaven was opened, and the ark of the covenant of the Lord was seen in His temple. And there were lightnings, noises, thunderings and huge hail.

< Ufunuo 11 >