< Ufunuo 11 >
1 Ndipo nikapewa mwanzi uliokuwa kama ufito wa kupimia, nikaambiwa, “Nenda ukapime hekalu la Mungu pamoja na madhabahu, nawe uwahesabu wale waabuduo humo.
And there was given me a reed like unto a rod: and it was said to me: Arise, and measure the temple of God, and the altar and them that adore therein.
2 Lakini usiupime ua wa nje wa Hekalu, uache, kwa sababu ua huo wamepewa watu wa Mataifa. Hao wataukanyagakanyaga mji mtakatifu kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
But the court, which is without the temple, cast out, and measure it not: because it is given unto the Gentiles, and the holy city they shall tread under foot two and forty months:
3 Nami nitawapa mashahidi wangu wawili uwezo, nao watoe unabii kwa muda wa siku 1,260, wakiwa wamevaa nguo za gunia.”
And I will give unto my two witnesses, and they shall prophesy a thousand two hundred sixty days, clothed in sackcloth.
4 Hawa ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili vya taa visimamavyo mbele za Bwana Mungu wa dunia yote.
These are the two olive trees, and the two candlesticks, that stand before the Lord of the earth.
5 Kama mtu yeyote akitaka kuwadhuru, moto hutoka vinywani mwao na kuwateketeza adui zao. Hivi ndivyo impasavyo kufa mtu yeyote atakayetaka kuwadhuru.
And if any man will hurt them, fire shall come out of their mouths, and shall devour their enemies. And if any man will hurt them, in this manner must he be slain.
6 Watu hawa wanao uwezo wa kufunga anga ili mvua isinyeshe wakati wote watakapokuwa wanatoa unabii wao. Nao watakuwa na uwezo wa kuyabadili maji kuwa damu na kuipiga dunia kwa kila aina ya mapigo mara kwa mara kama watakavyo.
These have power to shut heaven, that it rain not in the days of their prophecy: and they have power over waters to turn them into blood, and to strike the earth with all plagues as often as they will.
7 Basi watakapokuwa wamemaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika lile Shimo atapigana nao vita, atawashinda na kuwaua. (Abyssos )
And when they shall have finished their testimony, the beast, that ascendeth out of the abyss, shall make war against them, and shall overcome them, and kill them. (Abyssos )
8 Maiti zao zitabaki katika barabara ya mji mkubwa, ambao kwa fumbo unaitwa Sodoma na Misri, ambapo pia Bwana wao alisulubiwa.
And their bodies shall lie in the streets of the great city, which is called spiritually, Sodom and Egypt, where their Lord also was crucified.
9 Kwa muda wa siku tatu na nusu, watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa wataziangalia hizo maiti zao na hawataruhusu wazikwe.
And they of the tribes, and peoples, and tongues, and nations, shall see their bodies for three days and a half: and they shall not suffer their bodies to be laid in sepulchres.
10 Watu waishio duniani watazitazama kwa furaha maiti za hao manabii wawili na kushangilia kwa kupeana zawadi kwa sababu hao manabii waliwatesa watu waishio duniani.
And they that dwell upon the earth shall rejoice over them, and make merry: and shall send gifts one to another, because these two prophets tormented them that dwelt upon the earth.
11 Lakini baada ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu ikawaingia, nao wakasimama kwa miguu yao na wote waliowaona wakaingiwa na hofu kuu.
And after three days and a half, the spirit of life from God entered into them. And they stood upon their feet, and great fear fell upon them that saw them.
12 Kisha wale manabii wawili wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, “Njooni huku juu!” Nao wakapaa mbinguni katika wingu, wakati adui zao wakiwa wanawatazama.
And they heard a great voice from heaven, saying to them: Come up hither. And they went up to heaven in a cloud: and their enemies saw them.
13 Saa iyo hiyo, kukatokea tetemeko kubwa la nchi na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka. Watu elfu saba wakauawa katika tetemeko hilo, nao walionusurika wakaogopa sana, wakamtukuza Mungu wa mbinguni.
And at that hour there was made a great earthquake, and the tenth part of the city fell: and there were slain in the earthquake names of men seven thousand: and the rest were cast into a fear, and gave glory to the God of heaven.
14 Ole ya pili imekwisha kupita, tazama ole ya tatu inakuja upesi.
The second woe is past: and behold the third woe will come quickly.
15 Yule malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake, pakawa na sauti kubwa mbinguni iliyosema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala milele na milele.” (aiōn )
And the seventh angel sounded the trumpet: and there were great voices in heaven, saying: The kingdom of this world is become our Lord’s and his Christ’s, and he shall reign for ever and ever. Amen. (aiōn )
16 Nao wale wazee ishirini na wanne, waliokuwa wameketi mbele za Mungu, kwenye viti vyao vya enzi, wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu,
And the four and twenty ancients, who sit on their seats in the sight of God, fell on their faces and adored God, saying:
17 wakisema: “Tunakushukuru, Bwana Mungu Mwenyezi, uliyeko na uliyekuwako, kwa kuwa umetwaa uweza wako mkuu na ukaanza kutawala.
We give thee thanks, O Lord God Almighty, who art, and who wast, and who art to come: because thou hast taken to thee thy great power, and thou hast reigned.
18 Mataifa walikasirika nao wakati wa ghadhabu yako umewadia. Wakati umewadia wa kuwahukumu waliokufa na kuwapa thawabu watumishi wako manabii na watakatifu wako pamoja na wale wote wanaoliheshimu Jina lako, wakubwa kwa wadogo: na kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.”
And the nations were angry, and thy wrath is come, and the time of the dead, that they should be judged, and that thou shouldest render reward to thy servants the prophets and the saints, and to them that fear thy name, little and great, and shouldest destroy them who have corrupted the earth.
19 Ndipo hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana humo ndani. Kukatokea mianga ya umeme wa radi, ngurumo, sauti za radi, tetemeko la nchi na mvua kubwa ya mawe.
And the temple of God was opened in heaven: and the ark of his testament was seen in his temple, and there were lightnings, and voices, and an earthquake, and great hail.