< Ufunuo 10 >

1 Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulingʼaa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto.
And I saw another, a mighty messenger, descending out of heaven, —arrayed with a cloud, and, the rainbow, was upon his head, and, his face, was as the sun, and, his feet, were as pillars of fire,
2 Mkononi mwake alikuwa ameshika kijitabu kilichokuwa kimefunguliwa. Akauweka mguu wake wa kuume juu ya bahari na mguu wake wa kushoto akauweka juu ya nchi kavu.
and [he was] holding in his hand a little scroll, opened; and he set his right foot upon the sea, and his left upon the land,
3 Naye akapiga kelele kwa sauti kuu kama simba anayenguruma. Alipopiga kelele, zile radi saba zikatoa ngurumo zake.
and cried out with a loud voice, just as a lion, roareth. And, when he cried out, the seven thunders uttered their own voices.
4 Nazo zile radi saba zilipotoa ngurumo, nilitaka kuanza kuandika, lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Yatie muhuri hayo yaliyosemwa na hizo radi saba na usiyaandike.”
And, when the seven thunders had spoken, I was about to write, and I heard a voice out of heaven, saying—Seal up the things which the seven thunders have uttered, and do not write, them.
5 Kisha yule malaika niliyekuwa nimemwona akiwa amesimama juu ya bahari na juu ya nchi akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni.
And, the messenger, whom I saw standing upon the sea and upon the land, lifted up his right hand unto heaven,
6 Naye akaapa kwa Yule aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote viijazavyo, pamoja na bahari na vyote vilivyomo ndani yake, akasema, “Hakuna kungoja tena! (aiōn g165)
and sware, by him that liveth unto the ages of ages, who created heaven, and the things that are therein, and the earth, and the things that are therein, [and the sea, and the things that are therein, ] Delay, no longer, shall there be; (aiōn g165)
7 Lakini katika siku zile ambazo huyo malaika wa saba atakapokaribia kuipiga hiyo tarumbeta yake, siri ya Mungu itatimizwa, kama vile alivyowatangazia watumishi wake manabii.”
but, in the days of the sounding of the seventh messenger, as soon as he is about to blow his trumpet, then shall have been completed the sacred secret of God as he told the good-news unto his own servants the prophets.
8 Ndipo ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni ikasema nami tena ikaniambia, “Nenda, chukua kile kitabu kilichofunguliwa kilichoko mkononi mwa yule malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
And, the voice which I had heard out of heaven, [I] again [heard] talking with me; and saying—Go take the opened scroll, that is in the hand of the messenger who is standing upon the sea and upon the land.
9 Basi nikamwendea nikamwomba yule malaika anipe kile kitabu kidogo. Akaniambia, “Chukua na ukile. Kitakuwa kichungu tumboni mwako, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.”
And I went away unto the messenger, asking him to give me the little scroll; and he saith unto me—Take it, and eat it up; and it shall embitter thy belly, but, in thy mouth, shall be sweet as honey.
10 Hivyo nikakichukua kile kitabu kidogo kutoka mkononi mwa yule malaika nikakila. Kilikuwa kitamu kama asali kinywani mwangu, lakini baada ya kukila, tumbo langu likatiwa uchungu.
And I took the little scroll out of the hand of the messenger, and did eat it up; and it was, in my mouth, as honey, sweet, and, when I had eaten it, embittered was my belly.
11 Kisha nikaambiwa, “Imekupasa kutoa unabii tena kuhusu makabila mengi, mataifa, lugha na wafalme.”
And they say unto me—It behoveth thee again to prophesy against peoples and nations and tongues, and many kings.

< Ufunuo 10 >