< Ufunuo 10 >
1 Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulingʼaa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto.
And I saw another mighty angel coming down out of heaven, clad with a cloud; and a rainbow was upon his head, and his face was like the sun, and his feet like pillars of fire.
2 Mkononi mwake alikuwa ameshika kijitabu kilichokuwa kimefunguliwa. Akauweka mguu wake wa kuume juu ya bahari na mguu wake wa kushoto akauweka juu ya nchi kavu.
In his hand he had a little book, open; and he set his right foot upon the sea, and his left upon the land.
3 Naye akapiga kelele kwa sauti kuu kama simba anayenguruma. Alipopiga kelele, zile radi saba zikatoa ngurumo zake.
With a great voice he shouted as a lion roars; and when he shouted, the seven thunders uttered their voices.
4 Nazo zile radi saba zilipotoa ngurumo, nilitaka kuanza kuandika, lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Yatie muhuri hayo yaliyosemwa na hizo radi saba na usiyaandike.”
When the seven thunders uttered their voices, I was about to write; but I heard a voice from the sky, saying, "Seal up the words which the seven thunders uttered, and write them not."
5 Kisha yule malaika niliyekuwa nimemwona akiwa amesimama juu ya bahari na juu ya nchi akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni.
And the angel whom I had seen standing upon the sea and upon the land lifted up his right hand to heaven,
6 Naye akaapa kwa Yule aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote viijazavyo, pamoja na bahari na vyote vilivyomo ndani yake, akasema, “Hakuna kungoja tena! (aiōn )
and swore by him who lives forever and ever, who created the heaven and all that is in it, and the earth and all that is in it, and the sea and all that is in it, "Delay there shall be no more, (aiōn )
7 Lakini katika siku zile ambazo huyo malaika wa saba atakapokaribia kuipiga hiyo tarumbeta yake, siri ya Mungu itatimizwa, kama vile alivyowatangazia watumishi wake manabii.”
but in the days of the voice of the seventh angel, when he is about to blow his trumpet, then shall there be finished the mystery of God, according to the Good News which he told unto his slaves, the prophets."
8 Ndipo ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni ikasema nami tena ikaniambia, “Nenda, chukua kile kitabu kilichofunguliwa kilichoko mkononi mwa yule malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
And the voice which I had heard from heaven, I heard again, speaking to me, and saying, "Go, take the little book that is open in the hand of the angel who stands upon the sea and upon the land."
9 Basi nikamwendea nikamwomba yule malaika anipe kile kitabu kidogo. Akaniambia, “Chukua na ukile. Kitakuwa kichungu tumboni mwako, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.”
And I went to the angel and told him to give me the little book. And he said to me. "Take it, and eat it up; it will make your belly bitter, but in your mouth it will be as sweet as honey."
10 Hivyo nikakichukua kile kitabu kidogo kutoka mkononi mwa yule malaika nikakila. Kilikuwa kitamu kama asali kinywani mwangu, lakini baada ya kukila, tumbo langu likatiwa uchungu.
I took the little book out of the hand of the angel, and ate it up, and it was in my mouth sweet like honey; but when I had eaten it, my belly was made bitter.
11 Kisha nikaambiwa, “Imekupasa kutoa unabii tena kuhusu makabila mengi, mataifa, lugha na wafalme.”
Then I was told, "You must prophesy again over many peoples and nations and tongues and kings."