< Ufunuo 1 >

1 Ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa na Mungu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo ni lazima yatukie hivi karibuni. Alijulisha mambo haya kwa kumtuma malaika wake kwa Yohana mtumishi wake,
yat prakAzitaM vAkyam IzvaraH svadAsAnAM nikaTaM zIghramupasthAsyantInAM ghaTanAnAM darzanArthaM yIzukhrISTe samarpitavAn tat sa svIyadUtaM preSya nijasevakaM yohanaM jJApitavAn|
2 ambaye anashuhudia kuhusu kila kitu alichokiona, yaani, Neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo.
sa cezvarasya vAkye khrISTasya sAkSye ca yadyad dRSTavAn tasya pramANaM dattavAn|
3 Amebarikiwa yeye asomaye maneno ya unabii huu, na wamebarikiwa wale wanaoyasikia na kuyatia moyoni yale yaliyoandikwa humo, kwa sababu wakati umekaribia.
etasya bhaviSyadvaktRgranthasya vAkyAnAM pAThakaH zrotArazca tanmadhye likhitAjJAgrAhiNazca dhanyA yataH sa kAlaH sannikaTaH|
4 Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia: Neema na amani iwe kwenu kutoka kwake aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, na kutoka kwa wale roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi,
yohan AziyAdezasthAH sapta samitIH prati patraM likhati| yo varttamAno bhUto bhaviSyaMzca ye ca saptAtmAnastasya siMhAsanasya sammukhe tiSThanti
5 na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni yule shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, mtawala wa wafalme wa dunia. Kwake yeye anayetupenda na ambaye ametuweka huru kutoka dhambi zetu kwa damu yake,
yazca yIzukhrISTo vizvastaH sAkSI mRtAnAM madhye prathamajAto bhUmaNDalastharAjAnAm adhipatizca bhavati, etebhyo 'nugrahaH zAntizca yuSmAsu varttatAM|
6 akatufanya sisi kuwa ufalme na makuhani, tumtumikie Mungu wake ambaye ni Baba yake. Utukufu na uwezo ni vyake milele na milele! Amen. (aiōn g165)
yo 'smAsu prItavAn svarudhireNAsmAn svapApebhyaH prakSAlitavAn tasya piturIzvarasya yAjakAn kRtvAsmAn rAjavarge niyuktavAMzca tasmin mahimA parAkramazcAnantakAlaM yAvad varttatAM| Amen| (aiōn g165)
7 Tazama! Anakuja na mawingu, na kila jicho litamwona, hata wale waliomchoma; na makabila yote duniani yataomboleza kwa sababu yake. Naam, ndivyo itakavyokuwa! Amen.
pazyata sa meghairAgacchati tenaikaikasya cakSustaM drakSyati ye ca taM viddhavantaste 'pi taM vilokiSyante tasya kRte pRthivIsthAH sarvve vaMzA vilapiSyanti| satyam Amen|
8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.”
varttamAno bhUto bhaviSyaMzca yaH sarvvazaktimAn prabhuH paramezvaraH sa gadati, ahameva kaH kSazcArthata Adirantazca|
9 Mimi, Yohana, ndugu yenu ninayeshiriki pamoja nanyi mateso katika Yesu na katika ufalme na uvumilivu katika saburi, nilikuwa katika kisiwa cha Patmo kwa ajili ya neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu.
yuSmAkaM bhrAtA yIzukhrISTasya klezarAjyatitikSANAM sahabhAgI cAhaM yohan Izvarasya vAkyaheto ryIzukhrISTasya sAkSyahetozca pAtmanAmaka upadvIpa AsaM|
10 Katika siku ya Bwana, nilikuwa katika Roho na nikasikia sauti kubwa kama ya baragumu nyuma yangu
tatra prabho rdine AtmanAviSTo 'haM svapazcAt tUrIdhvanivat mahAravam azrauSaM,
11 ikisema, “Andika kwenye kitabu haya yote unayoyaona, kisha uyapeleke kwa makanisa saba, yaani: Efeso, Smirna, Pergamo, Thiatira, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”
tenoktam, ahaM kaH kSazcArthata Adirantazca| tvaM yad drakSyasi tad granthe likhitvAziyAdezasthAnAM sapta samitInAM samIpam iphiSaM smurNAM thuyAtIrAM sArddiM philAdilphiyAM lAyadIkeyAJca preSaya|
12 Ndipo nikageuka ili nione ni sauti ya nani iliyokuwa ikisema nami. Nami nilipogeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu,
tato mayA sambhASamANasya kasya ravaH zrUyate taddarzanArthaM mukhaM parAvarttitaM tat parAvartya svarNamayAH sapta dIpavRkSA dRSTAH|
13 na katikati ya vile vinara vya taa, alikuwamo mtu kama Mwana wa Adamu, akiwa amevaa joho refu, na mkanda wa dhahabu ukiwa umefungwa kifuani mwake.
teSAM sapta dIpavRkSANAM madhye dIrghaparicchadaparihitaH suvarNazRGkhalena veSTitavakSazca manuSyaputrAkRtireko janastiSThati,
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu, nyeupe kama theluji, nayo macho yake yalikuwa kama mwali wa moto.
tasya ziraH kezazca zvetameSalomAnIva himavat zretau locane vahnizikhAsame
15 Nyayo zake zilikuwa kama shaba inayongʼaa, katika tanuru ya moto, nayo sauti yake ilikuwa kama mugurumo ya maji mengi.
caraNau vahnikuNDetApitasupittalasadRzau ravazca bahutoyAnAM ravatulyaH|
16 Katika mkono wake wa kuume alishika nyota saba, na kinywani mwake ulitoka upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa kama jua likingʼaa kwa nguvu zake zote.
tasya dakSiNahaste sapta tArA vidyante vaktrAcca tIkSNo dvidhAraH khaGgo nirgacchati mukhamaNDalaJca svatejasA dedIpyamAnasya sUryyasya sadRzaM|
17 Nilipomwona, nilianguka miguuni pake kama aliyekufa. Ndipo akauweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope, Mimi ndiye wa Kwanza na wa Mwisho.
taM dRSTvAhaM mRtakalpastaccaraNe patitastataH svadakSiNakaraM mayi nidhAya tenoktam mA bhaiSIH; aham Adirantazca|
18 Mimi ni Yeye Aliye Hai, niliyekuwa nimekufa, na tazama, ni hai milele na milele! Nami ninazo funguo za mauti na kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
aham amarastathApi mRtavAn kintu pazyAham anantakAlaM yAvat jIvAmi| Amen| mRtyoH paralokasya ca kuJjikA mama hastagatAH| (aiōn g165, Hadēs g86)
19 “Basi andika mambo uliyoyaona, yaliyopo na yale yatakayotukia baada ya haya.
ato yad bhavati yaccetaH paraM bhaviSyati tvayA dRSTaM tat sarvvaM likhyatAM|
20 Kuhusu siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume na vile vinara saba vya taa vya dhahabu ni hii: Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, navyo vile vinara saba ni hayo makanisa saba.
mama dakSiNahaste sthitA yAH sapta tArA ye ca svarNamayAH sapta dIpavRkSAstvayA dRSTAstattAtparyyamidaM tAH sapta tArAH sapta samitInAM dUtAH suvarNamayAH sapta dIpavRkSAzca sapta samitayaH santi|

< Ufunuo 1 >