< Ufunuo 1 >

1 Ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa na Mungu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo ni lazima yatukie hivi karibuni. Alijulisha mambo haya kwa kumtuma malaika wake kwa Yohana mtumishi wake,
C'est ici la Révélation de Jésus-Christ, que Dieu lui a donnée pour montrer à ses serviteurs les choses qui doivent arriver bientôt, qu'il a envoyée et fait connaître par son ange à son serviteur Jean,
2 ambaye anashuhudia kuhusu kila kitu alichokiona, yaani, Neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo.
lequel a rendu témoignage à la parole de Dieu et au témoignage de Jésus-Christ, sur tout ce qu'il a vu.
3 Amebarikiwa yeye asomaye maneno ya unabii huu, na wamebarikiwa wale wanaoyasikia na kuyatia moyoni yale yaliyoandikwa humo, kwa sababu wakati umekaribia.
Heureux celui qui lit et ceux qui entendent les paroles de la prophétie, et qui gardent les choses qui y sont écrites, car le temps est proche.
4 Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia: Neema na amani iwe kwenu kutoka kwake aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, na kutoka kwa wale roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi,
Jean, aux sept assemblées qui sont en Asie: Grâce et paix à vous de la part de Dieu, qui est, qui était et qui vient, et des sept Esprits qui sont devant son trône,
5 na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni yule shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, mtawala wa wafalme wa dunia. Kwake yeye anayetupenda na ambaye ametuweka huru kutoka dhambi zetu kwa damu yake,
et de la part de Jésus-Christ, le témoin fidèle, le premier-né d'entre les morts, et le chef des rois de la terre. À celui qui nous aime, qui nous a lavés de nos péchés par son sang -
6 akatufanya sisi kuwa ufalme na makuhani, tumtumikie Mungu wake ambaye ni Baba yake. Utukufu na uwezo ni vyake milele na milele! Amen. (aiōn g165)
et qui a fait de nous un Royaume, des prêtres pour son Dieu et Père - à lui la gloire et la domination pour les siècles des siècles. Amen. (aiōn g165)
7 Tazama! Anakuja na mawingu, na kila jicho litamwona, hata wale waliomchoma; na makabila yote duniani yataomboleza kwa sababu yake. Naam, ndivyo itakavyokuwa! Amen.
Voici, il vient sur les nuées, et tout œil le verra, même ceux qui l'ont percé. Toutes les tribus de la terre se lamenteront sur lui. Ainsi soit-il, Amen.
8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.”
« Je suis l'Alpha et l'Oméga, dit le Seigneur Dieu qui est, qui était et qui vient, le Tout-Puissant. »
9 Mimi, Yohana, ndugu yenu ninayeshiriki pamoja nanyi mateso katika Yesu na katika ufalme na uvumilivu katika saburi, nilikuwa katika kisiwa cha Patmo kwa ajili ya neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu.
Moi, Jean, votre frère et votre associé dans l'oppression, le Royaume et la persévérance en Jésus-Christ, j'étais sur l'île qu'on appelle Patmos, à cause de la Parole de Dieu et du témoignage de Jésus-Christ.
10 Katika siku ya Bwana, nilikuwa katika Roho na nikasikia sauti kubwa kama ya baragumu nyuma yangu
J'étais en Esprit au jour du Seigneur, et j'entendis derrière moi une voix forte, comme une trompette
11 ikisema, “Andika kwenye kitabu haya yote unayoyaona, kisha uyapeleke kwa makanisa saba, yaani: Efeso, Smirna, Pergamo, Thiatira, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”
qui disait: « Ce que tu vois, écris-le dans un livre et envoie-le aux sept assemblées: à Éphèse, à Smyrne, à Pergame, à Thyatire, à Sardes, à Philadelphie et à Laodicée. »
12 Ndipo nikageuka ili nione ni sauti ya nani iliyokuwa ikisema nami. Nami nilipogeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu,
Je me suis retourné pour voir la voix qui me parlait. Et je me retournai, et je vis sept chandeliers d'or.
13 na katikati ya vile vinara vya taa, alikuwamo mtu kama Mwana wa Adamu, akiwa amevaa joho refu, na mkanda wa dhahabu ukiwa umefungwa kifuani mwake.
Et parmi les chandeliers, il y en avait un qui ressemblait à un fils d'homme, vêtu d'une robe qui lui descendait jusqu'aux pieds, et d'une ceinture d'or autour de sa poitrine.
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu, nyeupe kama theluji, nayo macho yake yalikuwa kama mwali wa moto.
Sa tête et ses cheveux étaient blancs comme de la laine blanche, comme de la neige. Ses yeux étaient comme une flamme de feu.
15 Nyayo zake zilikuwa kama shaba inayongʼaa, katika tanuru ya moto, nayo sauti yake ilikuwa kama mugurumo ya maji mengi.
Ses pieds étaient semblables à de l'airain poli, comme s'il avait été affiné dans une fournaise. Sa voix était comme le bruit des grandes eaux.
16 Katika mkono wake wa kuume alishika nyota saba, na kinywani mwake ulitoka upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa kama jua likingʼaa kwa nguvu zake zote.
Il avait sept étoiles dans sa main droite. De sa bouche sortait une épée aiguë à deux tranchants. Son visage était comme le soleil brillant à son plus haut degré.
17 Nilipomwona, nilianguka miguuni pake kama aliyekufa. Ndipo akauweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope, Mimi ndiye wa Kwanza na wa Mwisho.
Quand je le vis, je tombai à ses pieds comme un mort. Il posa sa main droite sur moi, en disant: « N'aie pas peur. Je suis le premier et le dernier,
18 Mimi ni Yeye Aliye Hai, niliyekuwa nimekufa, na tazama, ni hai milele na milele! Nami ninazo funguo za mauti na kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
et le Vivant. J'étais mort, et voici que je suis vivant pour les siècles des siècles. Amen. J'ai les clés de la mort et du séjour des morts. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 “Basi andika mambo uliyoyaona, yaliyopo na yale yatakayotukia baada ya haya.
Écris donc les choses que tu as vues, les choses qui sont, et les choses qui arriveront dans la suite.
20 Kuhusu siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume na vile vinara saba vya taa vya dhahabu ni hii: Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, navyo vile vinara saba ni hayo makanisa saba.
Voici le mystère des sept étoiles que tu as vues dans ma main droite, et des sept chandeliers d'or: Les sept étoiles sont les anges des sept assemblées. Les sept chandeliers sont les sept assemblées.

< Ufunuo 1 >