< Ufunuo 1 >

1 Ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa na Mungu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo ni lazima yatukie hivi karibuni. Alijulisha mambo haya kwa kumtuma malaika wake kwa Yohana mtumishi wake,
The Revelation of Jesus Christ, which God gave unto Him, to shew to his servants things which must shortly come to pass; and He sent and signified it by his angel to his servant John,
2 ambaye anashuhudia kuhusu kila kitu alichokiona, yaani, Neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo.
who bare witness to the word of God and the testimony of Jesus Christ, and to whatever He saw.
3 Amebarikiwa yeye asomaye maneno ya unabii huu, na wamebarikiwa wale wanaoyasikia na kuyatia moyoni yale yaliyoandikwa humo, kwa sababu wakati umekaribia.
Happy is he that readeth, and those that hear the words of the prophecy, and keep the things that are written therein: for the time is near.
4 Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia: Neema na amani iwe kwenu kutoka kwake aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, na kutoka kwa wale roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi,
John to the seven churches in Asia---Grace and peace be to you, from Him who is, and who was, and who is to come; and from the seven Spirits which are before his throne;
5 na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni yule shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, mtawala wa wafalme wa dunia. Kwake yeye anayetupenda na ambaye ametuweka huru kutoka dhambi zetu kwa damu yake,
and from Jesus Christ, who is the faithful witness, the first-born from the dead, and the ruler of the kings of the earth. To Him that loved us, and washed us from our sins in his own blood,
6 akatufanya sisi kuwa ufalme na makuhani, tumtumikie Mungu wake ambaye ni Baba yake. Utukufu na uwezo ni vyake milele na milele! Amen. (aiōn g165)
and hath made us kings and priests to his God and Father, to Him be glory and dominion for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
7 Tazama! Anakuja na mawingu, na kila jicho litamwona, hata wale waliomchoma; na makabila yote duniani yataomboleza kwa sababu yake. Naam, ndivyo itakavyokuwa! Amen.
Behold, He is coming with the clouds, and every eye shall see Him, even they that pierced Him: and all the tribes of the earth shall lament before Him. Even so, Amen!
8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.”
I am the Alpha and the Omega, the beginning and the end, saith the Lord, who is, and who was, and who is to come, the Almighty.
9 Mimi, Yohana, ndugu yenu ninayeshiriki pamoja nanyi mateso katika Yesu na katika ufalme na uvumilivu katika saburi, nilikuwa katika kisiwa cha Patmo kwa ajili ya neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu.
I John, who am also your brother, and companion in the affliction, and in the kingdom and patience of Jesus Christ, was in the island called Patmos, for the sake of the word of God, and for the testimony of Jesus Christ.
10 Katika siku ya Bwana, nilikuwa katika Roho na nikasikia sauti kubwa kama ya baragumu nyuma yangu
Here I was in the Spirit on the Lord's-day: and heard behind me a loud voice, as of a trumpet,
11 ikisema, “Andika kwenye kitabu haya yote unayoyaona, kisha uyapeleke kwa makanisa saba, yaani: Efeso, Smirna, Pergamo, Thiatira, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”
saying, I am the Alpha and the Omega, the first and the last; and, What thou seest write in a book, and send it to the seven churches in Asia, to Ephesus, and to Smyrna, and to Pergamos, and to Thyatira, and to Sardis, and to Philadelphia, and to Laodicea.
12 Ndipo nikageuka ili nione ni sauti ya nani iliyokuwa ikisema nami. Nami nilipogeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu,
And I turned to see the voice that spake to me: and when I turned, I saw seven golden candlesticks;
13 na katikati ya vile vinara vya taa, alikuwamo mtu kama Mwana wa Adamu, akiwa amevaa joho refu, na mkanda wa dhahabu ukiwa umefungwa kifuani mwake.
and in the midst of the seven candlesticks one like the Son of man, clothed with a long robe, and girded about the breasts with a golden girdle.
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu, nyeupe kama theluji, nayo macho yake yalikuwa kama mwali wa moto.
His head and his hairs were white like white wool, as white as snow; and his eyes as a flame of fire;
15 Nyayo zake zilikuwa kama shaba inayongʼaa, katika tanuru ya moto, nayo sauti yake ilikuwa kama mugurumo ya maji mengi.
and his feet like fine brass, as if they were glowing in a furnace: and his voice as the sound of many waters:
16 Katika mkono wake wa kuume alishika nyota saba, na kinywani mwake ulitoka upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa kama jua likingʼaa kwa nguvu zake zote.
and He had in his right hand seven stars, and out of his mouth went a sharp two-edged sword: and his countenance was as the sun when he shineth in his strength.
17 Nilipomwona, nilianguka miguuni pake kama aliyekufa. Ndipo akauweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope, Mimi ndiye wa Kwanza na wa Mwisho.
And when I saw Him, I fell at his feet as dead; and He laid his right hand upon me, and said to me, "Fear not,
18 Mimi ni Yeye Aliye Hai, niliyekuwa nimekufa, na tazama, ni hai milele na milele! Nami ninazo funguo za mauti na kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
I am the first and the last, who live, though I was dead; and behold, I am alive for ever and ever, Amen, and have the keys of hades and of death. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 “Basi andika mambo uliyoyaona, yaliyopo na yale yatakayotukia baada ya haya.
Write what thou hast seen, the things which are, and which are to be hereafter."
20 Kuhusu siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume na vile vinara saba vya taa vya dhahabu ni hii: Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, navyo vile vinara saba ni hayo makanisa saba.
As to the mystery of the seven stars which thou sawest in my right hand, and the seven golden candlesticks; the seven stars are the angels of the seven churches, and the seven candlesticks which thou sawest are the seven churches.

< Ufunuo 1 >