< Zaburi 1 >

1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
خوشابحال کسی‌که به مشورت شریران نرود و به راه گناهکاران نایستد، و درمجلس استهزاکنندگان ننشیند؛۱
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
بلکه رغبت اودر شریعت خداوند است و روز و شب درشریعت او تفکر می‌کند.۲
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
پس مثل درختی نشانده نزد نهرهای آب خواهد بود، که میوه خودرا در موسمش می‌دهد، و برگش پژمرده نمی گردد و هر‌آنچه می‌کند نیک انجام خواهدبود.۳
4 Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
شریران چنین نیستند، بلکه مثل کاهند که بادآن را پراکنده می‌کند.۴
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
لهذا شریران در داوری نخواهند ایستاد و نه گناهکاران در جماعت عادلان.۵
6 Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.
زیرا خداوند طریق عادلان را می‌داند، ولی طریق گناهکاران هلاک خواهد شد.۶

< Zaburi 1 >