< Zaburi 1 >
1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
Heureux l’homme qui ne suit point les conseils des méchants, qui ne se tient pas dans la voie des pécheurs, et ne prend point place dans la société des railleurs,
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
mais qui trouve son plaisir dans la Loi de l’Eternel, et médite cette Loi jour et nuit!
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
Il sera comme un arbre planté auprès des cours d’eau, qui donne ses fruits en leur saison, et dont les feuilles ne se flétrissent point: tout ce qu’il fera réussira.
4 Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Tels ne sont pas les méchants, mais plutôt comme le chaume que pourchasse le vent.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Aussi les méchants n’ont-ils pas le dessus dans le jugement, ni les pécheurs dans l’assemblée des justes.
6 Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.
Car l’Eternel protège la voie des justes, mais la voie des méchants conduit à la ruine.