< Zaburi 1 >

1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
BOOK I HAPPY IS the man that hath not walked in the counsel of the wicked, nor stood in the way of sinners, nor sat in the seat of the scornful.
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
But his delight is in the law of the LORD; and in His law doth he meditate day and night.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
And he shall be like a tree planted by streams of water, that bringeth forth its fruit in its season, and whose leaf doth not wither; and in whatsoever he doeth he shall prosper.
4 Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Not so the wicked; but they are like the chaff which the wind driveth away.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Therefore the wicked shall not stand in the judgment, nor sinners in the congregation of the righteous.
6 Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.
For the LORD regardeth the way of the righteous; but the way of the wicked shall perish.

< Zaburi 1 >