< Zaburi 1 >

1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
Blessed is the man that walketh not in the counsel of the wicked, and standeth not in the way of sinners, and sitteth not in the seat of scorners;
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
But his delight is in Jehovah's law, and in his law doth he meditate day and night.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
And he [is] as a tree planted by brooks of water, which giveth its fruit in its season, and whose leaf fadeth not; and all that he doeth prospereth.
4 Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
The wicked are not so; but are as the chaff which the wind driveth away.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Therefore the wicked shall not stand in the judgment, nor sinners in the assembly of the righteous.
6 Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.
For Jehovah knoweth the way of the righteous, but the way of the wicked shall perish.

< Zaburi 1 >