< Zaburi 99 >

1 Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
RAB egemenlik sürüyor, titresin halklar! Keruvlar arasında tahtına oturmuş, Sarsılsın yeryüzü!
2 Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
RAB Siyon'da uludur, Yücedir O, bütün halklara egemendir.
3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
Övsünler büyük, müthiş adını! O kutsaldır.
4 Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
Ey adaleti seven güçlü kral, Eşitliği sen sağladın, Yakup soyunda doğru ve adil olanı sen yaptın.
5 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
Yüceltin Tanrımız RAB'bi, Ayaklarının taburesi önünde tapının! O kutsaldır.
6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
Musa'yla Harun O'nun kâhinlerindendi, Samuel de O'nu adıyla çağıranlar arasındaydı. RAB'be seslenirlerdi, O da yanıtlardı.
7 Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
Bulut sütunu içinden onlarla konuştu, Uydular O'nun buyruklarına, Kendilerine verdiği kurallara.
8 Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
Ya RAB Tanrımız, yanıt verdin onlara; Bağışlayıcı bir Tanrı oldun, Ama yaptıkları kötülüğü cezasız bırakmadın.
9 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.
Tanrımız RAB'bi yüceltin, Tapının O'na kutsal dağında! Çünkü Tanrımız RAB kutsaldır.

< Zaburi 99 >