< Zaburi 99 >
1 Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
¡Yahvé reina! Que tiemblen los pueblos. Se sienta entronizado entre los querubines. Que se mueva la tierra.
2 Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
Yahvé es grande en Sión. Está por encima de todos los pueblos.
3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
Que alaben tu nombre, grande y admirable. ¡Él es Santo!
4 Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
La fuerza del Rey también ama la justicia. Estableces la equidad. Tú ejecutas la justicia y la rectitud en Jacob.
5 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
Exalten a Yahvé, nuestro Dios. Adora a su escabel. ¡Él es Santo!
6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
Moisés y Aarón estaban entre sus sacerdotes, Samuel estaba entre los que invocan su nombre. Invocaron a Yahvé y éste les respondió.
7 Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
Les habló en la columna de nube. Guardaron sus testimonios, el estatuto que les dio.
8 Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
Tú les respondiste, Yahvé, nuestro Dios. Eres un Dios que los perdonó, aunque te hayas vengado de sus actos.
9 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.
Exalta a Yahvé, nuestro Dios. Adorar en su santa colina, porque Yahvé, nuestro Dios, es santo.