< Zaburi 99 >
1 Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
Gospod kraljuje; naj ljudstva trepetajo. On sedi med kerubi; naj bo zemlja omajana.
2 Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
Gospod je velik na Sionu; visoko je nad vsemi ljudstvi.
3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
Naj hvalijo tvoje veliko in strašno ime, kajti sveto je.
4 Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
Kraljeva moč ljubi tudi sodbo. Ti utrjuješ nepristranskost, izvršuješ sodbo in pravičnost v Jakobu.
5 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
Povišujte Gospoda, našega Boga in obožujte pri njegovi pručki, kajti on je svet.
6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
Mojzes in Aron med njegovimi duhovniki in Samuel med tistimi, ki kličejo njegovo ime; klicali so Gospoda in jim je odgovoril.
7 Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
Govoril jim je v oblačnem stebru; držali so se njegovih pričevanj in odredbe, ki jim jo je dal.
8 Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
Ti jim odgovarjaš, oh Gospod, naš Bog. Bil si jim Bog, ki odpušča, čeprav se maščuješ njihovim domiselnostim.
9 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.
Povišujte Gospoda, našega Boga in obožujte ga pri njegovi sveti gori, kajti Gospod, naš Bog, je svet.