< Zaburi 99 >

1 Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
יהוה מלך ירגזו עמים ישב כרובים תנוט הארץ׃
2 Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
יהוה בציון גדול ורם הוא על כל העמים׃
3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
יודו שמך גדול ונורא קדוש הוא׃
4 Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
ועז מלך משפט אהב אתה כוננת מישרים משפט וצדקה ביעקב אתה עשית׃
5 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
רוממו יהוה אלהינו והשתחוו להדם רגליו קדוש הוא׃
6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
משה ואהרן בכהניו ושמואל בקראי שמו קראים אל יהוה והוא יענם׃
7 Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
בעמוד ענן ידבר אליהם שמרו עדתיו וחק נתן למו׃
8 Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
יהוה אלהינו אתה עניתם אל נשא היית להם ונקם על עלילותם׃
9 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.
רוממו יהוה אלהינו והשתחוו להר קדשו כי קדוש יהוה אלהינו׃

< Zaburi 99 >