< Zaburi 99 >
1 Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
Psaume à David (de David) lui-même.
2 Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
Le Seigneur est grand dans Sion; il est élevé au-dessus de tous les peuples.
3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
Qu’ils rendent gloire à votre grand nom, parce qu’il est terrible et saint,
4 Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
Et que l’honneur d’un roi aime le jugement. Vous avez préparé des voies droites: jugement et justice dans Jacob, c’est vous qui les avez exercés.
5 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
Exaltez le Seigneur notre Dieu, et adorez l’escabeau de ses pieds, parce qu’il est saint.
6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
Moïse et Aaron parmi ses prêtres, et Samuel entre ceux qui invoquent son nom, Invoquaient le Seigneur, et le Seigneur les exauçait;
7 Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
C’est du milieu d’une colonne de nuée qu’il leur parlait.
8 Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
Seigneur notre Dieu, vous les exauciez: ô Dieu, vous leur avez été propice, mais en vous vengeant de toutes leurs inventions.
9 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.
Exaltez le Seigneur notre Dieu, adorez-le sur sa montagne sainte; parce qu’il est saint, le Seigneur notre Dieu.