< Zaburi 99 >
1 Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
L'Éternel règne, les peuples tremblent; Il est assis sur les Chérubins, la terre est ébranlée.
2 Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
L'Éternel est grand en Sion, et élevé au-dessus de tous les peuples:
3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
qu'ils chantent Ton nom grand et redoutable, Il est saint!
4 Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
et la force du Roi qui aime la justice! Tu as fondé l'équité, et créé en Jacob la justice et le droit.
5 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
Exaltez l'Éternel, notre Dieu, et vous prosternez sur le marchepied de son trône! Il est saint!
6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
Moïse et Aaron, ses Lévites, et Samuel qui invoquait son nom, implorèrent l'Éternel, et Il les exauça.
7 Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
Il leur parla dans la colonne de nuée; ils gardèrent ses commandements, et l'ordonnance qu'il leur avait donnée.
8 Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
Éternel, notre Dieu, tu les as exaucés; tu fus pour eux un Dieu qui pardonne, et un Dieu vengeur, à cause de leurs méfaits.
9 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.
Exaltez l'Éternel, notre Dieu, et prosternez-vous sur sa sainte montagne! Car Il est saint, l'Éternel, notre Dieu.