< Zaburi 99 >

1 Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
The Lord hath regned, puplis ben wrooth; thou that sittist on cherubyn, the erthe be moued.
2 Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
The Lord is greet in Sion; and hiy aboue alle puplis.
3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
Knouleche thei to thi greet name, for it is ferdful and hooli;
4 Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
and the onour of the king loueth doom. Thou hast maad redi dressyngis; thou hast maad doom and riytfulnesse in Jacob.
5 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
Enhaunse ye oure Lord God; and worschipe ye the stool of hise feet, for it is hooli.
6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
Moises and Aaron weren among hise preestis; and Samuel was among hem that inwardli clepen his name. Thei inwardli clepiden the Lord, and he herde hem;
7 Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
in a piler of cloude he spak to hem. Thei kepten hise witnessyngis; and the comaundement which he yaf to hem.
8 Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
Oure Lord God, thou herdist hem; God, thou were merciful to hem, and thou tokist veniaunce on al her fyndyngis.
9 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.
Enhaunse ye oure Lord God, and worschipe ye in his hooli hil; for oure Lord God is hooli.

< Zaburi 99 >