< Zaburi 99 >

1 Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
The LORD reigneth; let the peoples tremble: he sitteth upon the cherubim; let the earth be moved.
2 Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
The LORD is great in Zion; and he is high above all the peoples.
3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
Let them praise thy great and terrible name: holy is he.
4 Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
The king’s strength also loveth judgment; thou dost establish equity, thou executest judgment and righteousness in Jacob.
5 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
Exalt ye the LORD our God, and worship at his footstool: holy is he.
6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
Moses and Aaron among his priests, and Samuel among them that call on his name; they called upon the LORD, and he answered them.
7 Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
He spake unto them in the pillar of cloud: they kept his testimonies, and the statute that he gave them.
8 Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
Thou answeredst them, O LORD our God: thou wast a God that forgavest them, though thou tookest vengeance of their doings.
9 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.
Exalt ye the LORD our God, and worship at his holy hill; for the LORD our God is holy.

< Zaburi 99 >