< Zaburi 99 >
1 Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
The LORD reigneth, let the nations tremble! He sitteth between the cherubs, let the earth quake!
2 Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
Great is the LORD upon Zion; He is exalted over all the nations.
3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
Let men praise thy great and terrible name! It is holy.
4 Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
Let them declare the glory of the King who loveth justice! Thou hast established equity; Thou dost execute justice in Jacob!
5 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
Exalt ye Jehovah, our God, And bow yourselves down at his footstool! He is holy.
6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
Moses and Aaron, with his priests, And Samuel, who called upon his name, —They called upon the LORD, and he answered them.
7 Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
He spake to them in the cloudy pillar; They kept his commandments, And the ordinances which he gave them.
8 Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
Thou, O LORD, our God! didst answer them; Thou wast to them a forgiving God, Though thou didst punish their transgressions!
9 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.
Exalt the LORD, our God. And worship at his holy mountain! For the LORD, our God, is holy.