< Zaburi 99 >

1 Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
The Lord reigneth, let the people tremble: he sitteth betweene the Cherubims, let the earth be moued.
2 Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
The Lord is great in Zion, and he is high aboue all the people.
3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
They shall prayse thy great and fearefull Name (for it is holy)
4 Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
And the Kings power, that loueth iudgement: for thou hast prepared equitie: thou hast executed iudgement and iustice in Iaakob.
5 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
Exalt the Lord our God, and fall downe before his footestoole: for he is holy.
6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
Moses and Aaron were among his Priests, and Samuel among such as call vpon his Name: these called vpon the Lord, and he heard them.
7 Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
Hee spake vnto them in the cloudie pillar: they kept his testimonies, and the Lawe that he gaue them.
8 Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
Thou heardest them, O Lord our God: thou wast a fauourable God vnto them, though thou didst take vengeance for their inuentions.
9 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.
Exalt the Lord our God, and fall downe before his holy Mountaine: for the Lord our God is holy.

< Zaburi 99 >