< Zaburi 98 >
1 Zaburi. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, kwa maana ametenda mambo ya ajabu; kitanga chake cha kuume na mkono wake mtakatifu umemfanyia wokovu.
Un salmo. Cantad a Yahvé un cántico nuevo, porque ha hecho cosas maravillosas. Su mano derecha y su brazo santo han obrado la salvación para él.
2 Bwana ameufanya wokovu wake ujulikane na amedhihirisha haki yake kwa mataifa.
Yahvé ha dado a conocer su salvación. Ha mostrado abiertamente su justicia a la vista de las naciones.
3 Ameukumbuka upendo wake na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli; miisho yote ya dunia imeuona wokovu wa Mungu wetu.
Se ha acordado de su amorosa bondad y de su fidelidad hacia la casa de Israel. Todos los confines de la tierra han visto la salvación de nuestro Dios.
4 Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote, ipaze sauti kwa nyimbo za shangwe na vinanda;
¡Aclamad a Yahvé, toda la tierra! Estalla y canta de alegría, sí, ¡canta alabanzas!
5 mwimbieni Bwana kwa kinubi, kwa kinubi na sauti za kuimba,
Canten alabanzas a Yahvé con el arpa, con el arpa y la voz de la melodía.
6 kwa tarumbeta na mvumo wa baragumu za pembe za kondoo dume: shangilieni kwa furaha mbele za Bwana, aliye Mfalme.
Con trompetas y sonido de cuerno de carnero, hagan un ruido alegre ante el Rey, Yahvé.
7 Bahari na ivume na kila kiliomo ndani yake, dunia na wote wakaao ndani yake.
Que el mar ruja con su plenitud; el mundo y los que lo habitan.
8 Mito na ipige makofi, milima na iimbe pamoja kwa furaha,
Que los ríos aplaudan. Que las montañas canten juntas de alegría.
9 vyote na viimbe mbele za Bwana, kwa maana yuaja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia kwa haki na mataifa kwa haki.
Quecanten ante Yahvé, porque viene a juzgar la tierra. Él juzgará al mundo con justicia, y los pueblos con equidad.