< Zaburi 97 >

1 Bwana anatawala, nchi na ifurahi, visiwa vyote vishangilie.
耶和华作王!愿地快乐! 愿众海岛欢喜!
2 Mawingu na giza nene vinamzunguka, haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake cha enzi.
密云和幽暗在他的四围; 公义和公平是他宝座的根基。
3 Moto hutangulia mbele zake na huteketeza adui zake pande zote.
有烈火在他前头行, 烧灭他四围的敌人。
4 Umeme wake wa radi humulika dunia, nchi huona na kutetemeka.
他的闪电光照世界, 大地看见便震动。
5 Milima huyeyuka kama nta mbele za Bwana, mbele za Bwana wa dunia yote.
诸山见耶和华的面, 就是全地之主的面,便消化如蜡。
6 Mbingu zinatangaza haki yake, na mataifa yote huona utukufu wake.
诸天表明他的公义; 万民看见他的荣耀。
7 Wote waabuduo sanamu waaibishwa, wale wajisifiao sanamu: mwabuduni yeye, enyi miungu yote!
愿一切事奉雕刻的偶像、 靠虚无之神自夸的,都蒙羞愧。 万神哪,你们都当拜他。
8 Sayuni husikia na kushangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako, Ee Bwana.
耶和华啊,锡安听见你的判断就欢喜; 犹大的城邑也都快乐。
9 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, ndiwe Uliye Juu Sana kuliko dunia yote; umetukuka sana juu ya miungu yote.
因为你—耶和华至高,超乎全地; 你被尊崇,远超万神之上。
10 Wale wanaompenda Bwana na wauchukie uovu, kwa maana yeye hulinda maisha ya waaminifu wake na kuwaokoa kutoka mkononi mwa mwovu.
你们爱耶和华的,都当恨恶罪恶; 他保护圣民的性命, 搭救他们脱离恶人的手。
11 Nuru huangaza wenye haki na furaha kwa watu wanyofu wa moyo.
散布亮光是为义人; 预备喜乐是为正直人。
12 Furahini katika Bwana, ninyi mlio wenye haki, lisifuni jina lake takatifu.
你们义人当靠耶和华欢喜, 称谢他可记念的圣名。

< Zaburi 97 >