< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
Oh, haz una nueva canción al Señor; deja que toda la tierra haga melodía al Señor.
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Haz canciones al Señor, bendiciendo su nombre; da las buenas nuevas de su salvación día tras día.
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Hablen de su gloria a las naciones, y sus maravillas a todos los pueblos.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Porque el Señor es grande y muy digno de alabanza; es más temible que todos los demás dioses.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
Porque todos los dioses de las naciones son dioses falsos; pero el Señor hizo los cielos.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Alabanza y magnificencia delante de él; Honor y gloria; fuerte y justo es su lugar santo.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Dad a Jehová, oh familias de los pueblos, dad al Señor gloria y fortaleza.
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Da al Señor la gloria de su nombre; toma contigo una ofrenda y ven a su casa.
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Oh, adora al Señor en su hermoso santuario; ten miedo delante de él, toda la tierra.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Di entre las naciones: Jehová es rey; sí, el mundo está ordenado para que no se mueva; él será un juez justo de los pueblos.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Alégrense los cielos, y la tierra se alegre; que el mar truene con todas sus aguas;
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Alégrese el campo, y todo lo que está en él; sí, que todos los árboles del bosque rebosarán de alegría,
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
Delante del Señor, porque él ha venido; él ha venido para ser el juez de la tierra; la tierra será juzgada en justicia, y los pueblos con su verdad.

< Zaburi 96 >