< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
CANTAD á Jehová canción nueva; cantad á Jehová, toda la tierra.
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Cantad á Jehová, bendecid su nombre: anunciad de día en día su salud.
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Contad entre las gentes su gloria, en todos los pueblos sus maravillas.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Porque grande es Jehová, y digno de suprema alabanza; terrible sobre todos los dioses.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
Porque todos los dioses de los pueblos son ídolos: mas Jehová hizo los cielos.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Alabanza y magnificencia delante de él: fortaleza y gloria en su santuario.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Dad á Jehová, oh familias de los pueblos, dad á Jehová la gloria y la fortaleza.
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Dad á Jehová la honra debida á su nombre: tomad presentes, y venid á sus atrios.
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Encorvaos á Jehová en la hermosura de [su] santuario: temed delante de él, toda la tierra.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Decid en las gentes: Jehová reinó, también afirmó el mundo, no será conmovido: juzgará á los pueblos en justicia.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Alégrense los cielos, y gócese la tierra: brame la mar y su plenitud.
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Regocíjese el campo, y todo lo que en él está: entonces todos los árboles del bosque rebosarán de contento,
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
Delante de Jehová que vino: porque vino á juzgar la tierra. Juzgará al mundo con justicia, y á los pueblos con su verdad.

< Zaburi 96 >