< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
¡Canten a Yavé un canto nuevo! ¡Cante a Yavé toda la tierra!
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
¡Canten a Yavé, bendigan su Nombre! Anuncien de día en día su salvación.
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Proclamen su gloria entre las naciones, Entre todos los pueblos, sus maravillosas obras.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Porque grande es Yavé Y digno de suprema alabanza. Él debe ser temido por encima de todos los ʼelohim.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
Porque todos los ʼelohim de los pueblos son ídolos. Pero Yavé hizo los cielos.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Esplendor y majestad hay ante Él. Fortaleza y hermosura hay en su Santuario.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Tributen a Yavé, oh familias de los pueblos. Tributen a Yavé gloria y fortaleza.
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Tributen a Yavé la gloria debida a su Nombre. Lleven ofrenda y entren en sus patios.
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Adoren a Yavé en la hermosura de la santidad. Tiemble ante Él toda la tierra.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Digan entre las naciones: ¡Yavé reina! Ciertamente el mundo está firmemente establecido. No será conmovido. Él juzgará a los pueblos con equidad.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
¡Alégrense los cielos Y regocíjese la tierra! Brame el mar y todo lo que contiene.
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Exáltese el campo y todo lo que hay en él. Entonces todos los árboles del bosque cantarán con gozo
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
Delante de Yavé Quien viene, Porque viene a juzgar la tierra. Él juzgará al mundo con justicia Y a los pueblos con su fidelidad.

< Zaburi 96 >