< Zaburi 96 >
1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
Cante para Yahweh uma nova canção! Cantem para Yahweh, toda a terra.
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Cante para Yahweh! Bendito seja seu nome! Proclamar sua salvação de dia para dia!
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Declare sua glória entre as nações, suas obras maravilhosas entre todos os povos.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Para Yahweh é ótimo e muito louvável! Ele é para ser temido acima de todos os deuses.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
Pois todos os deuses dos povos são ídolos, mas Yahweh fez os céus.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
A honra e a majestade estão diante dele. A força e a beleza estão em seu santuário.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Atribuam a Yahweh, suas famílias de nações, atribuem a Yahweh glória e força.
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Atribua a Yahweh a glória devido a seu nome. Traga uma oferta, e venha a sua corte.
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Adorar a Yahweh em santa disposição. Treme diante dele, toda a terra.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Diga entre as nações: “Yahweh reina”. O mundo também está estabelecido. Não pode ser movido. Ele julgará os povos com equidade.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Que os céus se alegrem, e que a terra se regozije. Deixem o mar bramir, e sua plenitude!
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Let o campo e tudo o que há nele exultam! Então todas as árvores do bosque cantarão de alegria
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
antes de Yahweh; pois ele vem, pois ele vem para julgar a terra. Ele julgará o mundo com retidão, os povos com sua verdade.