< Zaburi 96 >
1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
KAKAULEKI on Ieowa kaul kap pot, jap karoj en kakauli on Ieowa!
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Kakaul on Ieowa o kapina mar a; padapadak jan eu ran lel eu duen a maur!
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Kajokajoi on men liki kan wau i, o on wei kan a manaman akan!
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Pwe Ieowa meid lapalap o meid kapinan, o meid kalom mon kot akan karoj.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
Pwe Kot en aramaj akan me mal a Ieowa kotin kapikadar lan akan.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Wau o linan mi mon jilan i, manaman o linan kin kadirela nan tanpaj a im jaraui.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Komail men liki kan, ki on Ieowa, ki on Ieowa linan o manaman.
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Komail ki on Ieowa linan en mar a; komail ko don mon japwilim a pera jaraui ianaki kijakij.
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Komail kaudoki on Ieowa ni omail kapwat jaraui, toun jappa karoj en majak i.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Komail kaireki on men liki kan: Ieowa ta Nanmarki! Pil jappa me teneten o jota pan mokimokid. A pan kotin kaunda kainok kan ni tiak pun.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Lan en peren kida, o jappa en popol; madau en nirnirjok o audepa!
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Jap en pereperen o audepa karoj, o tuka en nan wei karoj en nijinij.
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
On Ieowa, ni a kotido, ni a kotido, en kadeikada jappa. A pan kotin kaunda jappa ni tiak pun, o kainok kan ni a melel.