< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
Chantez à l'Éternel un cantique nouveau, chantez à l'Éternel, vous toutes les contrées!
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Chantez à l'Éternel, bénissez son nom, annoncez son salut de jour en jour!
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Racontez sa gloire parmi les nations, et ses merveilles parmi tous les peuples!
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Car Dieu est grand et digne d'une grande louange; Il est plus redoutable que tous les dieux;
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
car tous les dieux des peuples sont des idoles, et l'Éternel a fait les Cieux.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Devant sa face c'est splendeur et majesté, gloire et magnificence, dans son Sanctuaire.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Tribus des peuples, rendez à l'Éternel, rendez à l'Éternel l'honneur et la louange!
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Rendez à l'Éternel l'honneur dû à son nom! d Apportez des offrandes, et entrez dans ses parvis!
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Adorez l'Éternel avec une pompe sainte! Tremblez devant lui, vous toutes les contrées!
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Dites parmi les peuples: « L'Éternel règne; aussi le monde est ferme et ne chancelle point. Il juge les nations avec justice. »
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Que les Cieux se réjouissent, et que la terre tressaille; que la mer s'émeuve avec tout ce qu'elle enserre;
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
que les campagnes s'égaient avec tout ce qui les couvre; qu'ainsi les arbres des forêts frémissent tous d'allégresse
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
au devant de l'Éternel! Car Il vient, car il vient pour juger la terre. Il jugera le monde avec justice, et les peuples, selon sa vérité.

< Zaburi 96 >