< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
Chantez à Yahvé un chant nouveau! Chantez à Yahvé, toute la terre.
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Chantez à Yahvé! Bénissez son nom! Proclamez son salut au jour le jour!
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Déclarez sa gloire parmi les nations, ses merveilles parmi tous les peuples.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Car Yahvé est grand et très digne de louange! Il doit être craint par-dessus tous les dieux.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
Car tous les dieux des peuples sont des idoles, mais Yahvé a fait les cieux.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
L'honneur et la majesté sont devant lui. La force et la beauté sont dans son sanctuaire.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Rendez hommage à Yahvé, familles de nations, attribuer à Yahvé la gloire et la force.
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Rendez à Yahvé la gloire due à son nom. Apportez une offrande, et venez dans ses parvis.
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Adorez Yahvé avec des vêtements sacrés. Tremblez devant lui, toute la terre.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Dites parmi les nations: « Yahvé règne ». Le monde est également établi. Il ne peut pas être déplacé. Il jugera les peuples avec équité.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Que les cieux se réjouissent, et que la terre se réjouisse. Que la mer rugisse, et sa plénitude!
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Que le champ et tout ce qu'il contient exulte! Alors tous les arbres de la forêt chanteront de joie.
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
devant Yahvé, car il vient, car il vient pour juger la terre. Il jugera le monde avec justice, les peuples avec sa vérité.

< Zaburi 96 >