< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
Singe ye a newe song to the Lord; al erthe, synge ye to the Lord.
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Synge ye to the Lord, and blesse ye his name; telle ye his heelthe fro dai in to dai.
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Telle ye his glorie among hethene men; hise merueilis among alle puplis.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
For the Lord is greet, and worthi to be preisid ful myche; he is ferdful aboue alle goddis.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
For alle the goddis of hethene men ben feendis; but the Lord made heuenes.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Knouleching and fairnesse is in his siyt; hoolynesse and worthi doyng is in his halewing.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Ye cuntrees of hethene men, brynge to the Lord, bringe ye glorye and onour to the Lord;
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
bringe ye to the Lord glorie to hys name. Take ye sacrificis, and entre ye in to the hallis of hym;
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
herie ye the Lord in his hooli halle. Al erthe be moued of his face;
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
seie ye among hethene men, that the Lord hath regned. And he hath amendid the world, that schal not be moued; he schal deme puplis in equite.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Heuenes be glad, and the erthe make ful out ioye, the see and the fulnesse therof be moued togidere; feeldis schulen make ioye,
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
and alle thingis that ben in tho. Thanne alle the trees of wodis schulen make ful out ioye, for the face of the Lord, for he cometh;
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
for he cometh to deme the erthe. He schal deme the world in equite; and puplis in his treuthe.

< Zaburi 96 >