< Zaburi 96 >
1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
to sing to/for LORD song new to sing to/for LORD all [the] land: country/planet
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
to sing to/for LORD to bless name his to bear tidings from day to/for day salvation his
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
to recount in/on/with nation glory his in/on/with all [the] people to wonder his
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
for great: large LORD and to boast: praise much to fear: revere he/she/it upon all God
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
for all God [the] people idol and LORD heaven to make
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
splendor and glory to/for face: before his strength and beauty in/on/with sanctuary his
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
to give to/for LORD family people to give to/for LORD glory and strength
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
to give to/for LORD glory name his to lift: bear offering and to come (in): come to/for court his
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
to bow to/for LORD in/on/with adornment holiness to twist: tremble from face: before his all [the] land: country/planet
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
to say in/on/with nation LORD to reign also to establish: establish world not to shake to judge people in/on/with uprightness
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
to rejoice [the] heaven and to rejoice [the] land: country/planet to thunder [the] sea and fullness his
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
to exult field and all which in/on/with him then to sing all tree wood
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
to/for face: before LORD for to come (in): come for to come (in): come to/for to judge [the] land: country/planet to judge world in/on/with righteousness and people in/on/with faithfulness his