< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
O SING unto the LORD a new song: sing unto the LORD, all the earth.
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Sing unto the LORD, bless his name; shew forth his salvation from day to day.
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Declare his glory among the nations, his marvelous works among all the peoples.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
For great is the LORD, and highly to be praised: he is to be feared above all gods.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
For all the gods of the peoples are idols: but the LORD made the heavens.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Honour and majesty are before him: strength and beauty are in his sanctuary.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Give unto the LORD, ye kindreds of the peoples, give unto the LORD glory and strength.
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Give unto the LORD the glory due unto his name: bring an offering, and come into his courts.
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
O worship the LORD in the beauty of holiness: tremble before him, all the earth.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Say among the nations, The LORD reigneth: the world also is stablished that it cannot be moved: he shall judge the peoples with equity.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Let the heavens be glad, and let the earth rejoice; let the sea roar, and the fulness thereof;
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Let the field exult, and all that is therein; then shall all the trees of the wood sing for joy;
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
Before the LORD, for he cometh; for he cometh to judge the earth: he shall judge the world with righteousness, and the peoples with his truth.

< Zaburi 96 >