< Zaburi 96 >
1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
Sing to the Lord a new song, sing to the Lord, all the earth.
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Sing to the Lord, bless his name, from day to day herald his victory.
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Tell his glory among the nations, his wonders among all peoples.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
For great is the Lord and worthy all praise; held in awe, above all gods:
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
for all the gods of the nations are idols, but the Lord created the heavens.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Before him are splendor and majesty, beauty and strength in his holy place.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Ascribe to the Lord, you tribes of the nations, ascribe to the Lord glory and strength.
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Ascribe to the Lord the glory he manifests: bring you an offering, enter his courts.
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Bow to the Lord in holy array: tremble before him, all the earth.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Say to the nations, “The Lord is king.” The world stands firm to be shaken no more. He will judge the peoples with equity.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Let the heavens be glad and the earth rejoice, let the sea and its fulness thunder.
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Let the field, and all that is in it, exult; let the trees of the forest ring out their joy
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
before the Lord: for he comes, he comes to judge the earth. He will judge the world with justice and the nations with faithfulness.