< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
Sing to Adonai a new song! Sing to Adonai, all the earth.
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Sing to Adonai! Bless his name! Proclaim his yishu'ah ·salvation· from day to day!
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Declare his kavod ·weighty glory· among the nations, his marvelous works among all the peoples.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
For great is Adonai, and greatly to be praised! He is to be feared above all deities.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
For all the deities of the peoples are idols, but Adonai made the heavens.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Honor and majesty are before him. Strength and beauty are in his sanctuary.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Ascribe to Adonai, you families of nations, ascribe to Adonai kavod ·weighty glory· and strength.
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Ascribe to Adonai the kavod ·weighty glory· due to his name. Bring an offering, and come into his courts.
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Hawa ·Bow low, prostrate· to worship Adonai in holy array. Tremble before him, all the earth.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Say among the nations, “Adonai reigns.” The world is also established. It can’t be moved. He will judge the peoples with equity.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Let the heavens be glad, and let the earth rejoice. Let the sea roar, and its fullness!
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Let the field and all that is in it exult! Then all the trees of the woods shall sing for joy
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
before Adonai; for he comes, for he comes to judge the earth. He will judge the world with righteousness, the peoples with his truth.

< Zaburi 96 >