< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
Sing vnto the Lord a newe song: sing vnto the Lord, all the earth.
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Sing vnto the Lord, and prayse his Name: declare his saluation from day to day.
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Declare his glory among all nations, and his wonders among all people.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
For the Lord is great and much to be praysed: he is to be feared aboue all gods.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
For all the gods of the people are idoles: but the Lord made the heauens.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Strength and glory are before him: power and beautie are in his Sanctuarie.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Giue vnto the Lord, ye families of the people: giue vnto the Lord glory and power.
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Giue vnto the Lord the glory of his Name: bring an offering, and enter into his courtes.
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Worship the Lord in the glorious Sanctuarie: tremble before him all the earth.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Say among the nations, The Lord reigneth: surely the world shalbe stable, and not moue, and he shall iudge the people in righteousnesse.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Let the heauens reioyce, and let the earth be glad: let the sea roare, and all that therein is.
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Let the field be ioyfull, and all that is in it: let all the trees of the wood then reioyce
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
Before the Lord: for he commeth, for he cometh to iudge the earth: he wil iudge the world with righteousnes, and the people in his trueth.

< Zaburi 96 >