< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
Sing ye unto Jehovah a new song: sing unto Jehovah, all the earth.
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Sing unto Jehovah, bless his name; publish his salvation from day to day.
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Declare his glory among the nations, his wondrous works among all the peoples.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
For Jehovah is great and exceedingly to be praised; he is terrible above all gods.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
For all the gods of the peoples are idols; but Jehovah made the heavens.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Majesty and splendour are before him; strength and beauty are in his sanctuary.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Give unto Jehovah, ye families of peoples, give unto Jehovah glory and strength;
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Give unto Jehovah the glory of his name; bring an oblation and come into his courts;
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Worship Jehovah in holy splendour; tremble before him, all the earth.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Say among the nations, Jehovah reigneth! yea, the world is established, it shall not be moved; he will execute judgment upon the peoples with equity.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Let the heavens rejoice, and let the earth be glad; let the sea roar, and the fulness thereof;
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Let the field exult and all that is therein. Then shall all the trees of the forest sing for joy,
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
Before Jehovah, for he cometh; for he cometh to judge the earth: he will judge the world with righteousness, and the peoples in his faithfulness.

< Zaburi 96 >