< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
When the house was built after the Captivity, a Song of David. Sing to the Lord a new song; sing to the Lord, all the earth.
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Sing to the Lord, bless his name: proclaim his salvation from day to day.
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Publish his glory among the Gentiles, his wonderful works among all people.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
For the Lord is great, and greatly to be praised: he is terrible above all gods.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
For all the gods of the heathen are devils: but the Lord made the heavens.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Thanksgiving and beauty are before him: holiness and majesty are in his sanctuary.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Bring to the Lord, ye families of the Gentiles, bring to the Lord glory and honour.
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Bring to the Lord the glory [becoming] his name: take offerings, and go into his courts.
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Worship the Lord in his holy court: let all the earth tremble before him.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Say among the heathen, The Lord reigns: for he has established the world so that it shall not be moved: he shall judge the people in righteousness.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Let the heavens rejoice, and the earth exult; let the sea be moved, and the fullness of it.
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
The plains shall rejoice, and all things in them: then shall all the trees of the wood exult before the presence of the Lord:
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
for he comes, for he comes to judge the earth; he shall judge the world in righteousness, and the people with his truth.

< Zaburi 96 >