< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
Syng HERREN en ny sang, syng for Herren, al jorden,
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
syng for HERREN og lov hans Navn, fortæl om hans Frelse Dag efter Dag,
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
kundgør hans Ære blandt Folkene, hans Undere blandt alle Folkeslag!
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Thi stor og højlovet er HERREN, forfærdelig over alle Guder;
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
thi alle Folkeslagenes Guder er Afguder, HERREN er Himlens Skaber.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
For hans Åsyn er Højhed og Hæder, Lov og Pris i hans Helligdom.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Giv HERREN, I Folkeslags Slægter, giv HERREN Ære og Pris,
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
giv HERREN hans Navns Ære, bring Gaver og kom til hans Forgårde,
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
tilbed HERREN i helligt Skrud, bæv for hans Åsyn, al Jorden!
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Sig blandt Folkeslag: "HERREN har vist, han er Konge, han grundfæsted Jorden, den rokkes ikke, med Retfærd dømmer han Folkene."
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Himlen glæde sig, Jorden juble, Havet med dets Fylde bruse,
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Marken juble og alt, hvad den bærer! Da fryder sig alle Skovens Træer
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
for HERRENs Åsyn, thi han kommer, han kommer at dømme Jorden; han dømmer Jorden med Retfærd og Folkene i sin Trofasthed.

< Zaburi 96 >