< Zaburi 96 >
1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
Pjevajte Jahvi pjesmu novu! Pjevaj Jahvi, sva zemljo!
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Pjevajte Jahvi, hvalite ime njegovo! Navješćujte iz dana u dan spasenje njegovo,
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
kazujte poganima njegovu slavu, svim narodima čudesa njegova.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Velik je Jahve, hvale predostojan, strašniji od svih bogova!
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
Ništavni su svi bozi naroda. Jahve stvori nebesa!
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Slava je i veličanstvo pred njim, (sila) i sjaj u Svetištu njegovu.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Dajte Jahvi, narodna plemena, dajte Jahvi slavu i silu!
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Dajte Jahvi slavu imena njegova! Prinosite žrtvu i uđite u dvorove njegove,
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
poklonite se Jahvi u sjaju svetosti njegove. Strepi pred njim, zemljo sva!
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Nek' se govori među poganima: “Jahve kraljuje!” Svijet on učvrsti da se ne pomakne, narodima pravedno upravlja.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Raduj se, nebo, i kliči, zemljo! Neka huči more i što je u njemu!
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Nek' se raduje polje i što je na njemu, neka klikće šumsko drveće
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
pred Jahvom, jer dolazi, jer dolazi suditi zemlji. Sudit će svijetu u pravdi i narodima u istini svojoj.