< Zaburi 94 >

1 Ee Bwana, ulipizaye kisasi, Ee Mungu ulipizaye kisasi, uangaze sasa.
あだを報いられる神、主よ、あだを報いられる神よ、光を放ってください。
2 Ee Mhukumu wa dunia, inuka, uwalipize wenye kiburi kama wanavyostahili.
地をさばかれる者よ、立って高ぶる者にその受くべき罰をお与えください。
3 Hata lini, waovu, Ee Bwana, hata lini waovu watashangilia?
主よ、悪しき者はいつまで、悪しき者はいつまで勝ち誇るでしょうか。
4 Wanamimina maneno ya kiburi, watenda mabaya wote wamejaa majivuno.
彼らは高慢な言葉を吐き散らし、すべて不義を行う者はみずから高ぶります。
5 Ee Bwana, wanawaponda watu wako, wanawaonea urithi wako.
主よ、彼らはあなたの民を打ち砕き、あなたの嗣業を苦しめます。
6 Wanamchinja mjane na mgeni, na kuwaua yatima.
彼らはやもめと旅びとのいのちをうばい、みなしごを殺します。
7 Nao husema, “Bwana haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.”
彼らは言います、「主は見ない、ヤコブの神は悟らない」と。
8 Sikizeni, enyi wajinga miongoni mwa watu; enyi wapumbavu, lini mtakuwa na hekima?
民のうちの鈍き者よ、悟れ。愚かな者よ、いつ賢くなるだろうか。
9 Je, aliyeweka sikio asisikie? Aliyeumba jicho asione?
耳を植えた者は聞くことをしないだろうか、目を造った者は見ることをしないだろうか。
10 Je, anayeadhibisha mataifa asiadhibu? Je, awafundishaye wanadamu asiwe na maarifa?
もろもろの国民を懲らす者は罰することをしないだろうか、人を教える者は知識をもたないだろうか。
11 Bwana anajua mawazo ya mwanadamu; anajua kwamba ni ubatili.
主は人の思いの、むなしいことを知られる。
12 Ee Bwana, heri mtu anayeadhibishwa na wewe, mtu unayemfundisha kwa sheria yako,
主よ、あなたによって懲らされる人、あなたのおきてを教えられる人はさいわいです。
13 unampa utulivu siku za shida, mpaka shimo litakapokuwa limechimbwa kwa ajili ya mwovu.
あなたはその人を災の日からのがれさせ、悪しき者のために穴が掘られるまでその人に平安を与えられます。
14 Kwa kuwa Bwana hatawakataa watu wake, hatauacha urithi wake.
主はその民を捨てず、その嗣業を見捨てられないからです。
15 Hukumu itasimamishwa tena kwenye haki, wote walio na mioyo minyofu wataifuata.
さばきは正義に帰り、すべて心の正しい者はそれに従うでしょう。
16 Ni nani atakayeinuka dhidi ya mwovu kwa ajili yangu? Ni nani atakayenikinga dhidi ya watenda maovu?
だれがわたしのために立ちあがって、悪しき者を責めるだろうか。だれがわたしのために立って、不義を行う者を責めるだろうか。
17 Kama Bwana asingelinisaidia upesi, ningelikuwa ninaishi katika ukimya wa kifo.
もしも主がわたしを助けられなかったならば、わが魂はとくに音なき所に住んだであろう。
18 Niliposema, “Mguu wangu unateleza,” Ee Bwana, upendo wako ulinishikilia.
しかし「わたしの足がすべる」と思ったとき、主よ、あなたのいつくしみはわたしをささえられました。
19 Wakati wasiwasi ulipokuwa mwingi ndani yangu, faraja yako ilinipa furaha nafsini mwangu.
わたしのうちに思い煩いの満ちるとき、あなたの慰めはわが魂を喜ばせます。
20 Je, kiti cha utawala wa udhalimu kitajiunga nawe, ule utawala uletao taabu kutokana na sheria zake?
定めをもって危害をたくらむ悪しき支配者はあなたと親しむことができるでしょうか。
21 Huungana kuwashambulia wenye haki, kuwahukumu kufa wasio na hatia.
彼らは相結んで正しい人の魂を責め、罪のない者に死を宣告します。
22 Lakini Bwana amekuwa ngome yangu, na Mungu wangu amekuwa mwamba ninaoukimbilia.
しかし主はわが高きやぐらとなり、わが神はわが避け所の岩となられました。
23 Yeye atawalipa kwa ajili ya dhambi zao na atawaangamiza kwa ajili ya maovu yao; Bwana Mungu wetu atawaangamiza.
主は彼らの不義を彼らに報い、彼らをその悪のゆえに滅ぼされます。われらの神、主は彼らを滅ぼされます。

< Zaburi 94 >