< Zaburi 94 >
1 Ee Bwana, ulipizaye kisasi, Ee Mungu ulipizaye kisasi, uangaze sasa.
Sinä koston Jumala, Herra, sinä koston Jumala, ilmesty kirkkaudessa.
2 Ee Mhukumu wa dunia, inuka, uwalipize wenye kiburi kama wanavyostahili.
Nouse, maan tuomari, kosta ylpeille heidän tekonsa.
3 Hata lini, waovu, Ee Bwana, hata lini waovu watashangilia?
Kuinka kauan jumalattomat, Herra, kuinka kauan jumalattomat saavat riemuita?
4 Wanamimina maneno ya kiburi, watenda mabaya wote wamejaa majivuno.
Ne syytävät suustaan julkeita sanoja, ne röyhkeilevät, kaikki nuo väärintekijät.
5 Ee Bwana, wanawaponda watu wako, wanawaonea urithi wako.
Sinun kansaasi, Herra, he runtelevat, ja sinun perintöosaasi he rasittavat.
6 Wanamchinja mjane na mgeni, na kuwaua yatima.
He tappavat leskiä ja muukalaisia ja murhaavat orpoja.
7 Nao husema, “Bwana haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.”
Ja he sanovat: "Ei Herra sitä näe, ei Jaakobin Jumala sitä huomaa".
8 Sikizeni, enyi wajinga miongoni mwa watu; enyi wapumbavu, lini mtakuwa na hekima?
Ymmärtäkää, te kansan järjettömät, ja te tomppelit-milloin te tulette järkiinne?
9 Je, aliyeweka sikio asisikie? Aliyeumba jicho asione?
Joka on korvan istuttanut, hänkö ei kuulisi? Joka on silmän luonut, hänkö ei näkisi?
10 Je, anayeadhibisha mataifa asiadhibu? Je, awafundishaye wanadamu asiwe na maarifa?
Joka kansat kasvattaa, hänkö ei rankaisisi, hän, joka ihmisille opettaa tiedon?
11 Bwana anajua mawazo ya mwanadamu; anajua kwamba ni ubatili.
Herra tuntee ihmisten ajatukset; sillä he ovat kuin tuulen henkäys.
12 Ee Bwana, heri mtu anayeadhibishwa na wewe, mtu unayemfundisha kwa sheria yako,
Autuas se mies, jota sinä, Herra, kuritat ja jolle sinä opetat lakisi,
13 unampa utulivu siku za shida, mpaka shimo litakapokuwa limechimbwa kwa ajili ya mwovu.
antaaksesi hänelle rauhan pahoilta päiviltä, kunnes jumalattomalle on kaivettu hauta!
14 Kwa kuwa Bwana hatawakataa watu wake, hatauacha urithi wake.
Sillä Herra ei hylkää kansaansa eikä perintöosaansa heitä,
15 Hukumu itasimamishwa tena kwenye haki, wote walio na mioyo minyofu wataifuata.
vaan oikeus on vielä noudattava vanhurskautta, ja kaikki oikeamieliset seuraavat sitä.
16 Ni nani atakayeinuka dhidi ya mwovu kwa ajili yangu? Ni nani atakayenikinga dhidi ya watenda maovu?
Kuka nousee minun puolelleni pahoja vastaan, kuka asettuu minun rinnalleni väärintekijöitä vastaan?
17 Kama Bwana asingelinisaidia upesi, ningelikuwa ninaishi katika ukimya wa kifo.
Ellei Herra olisi minun apuni, pian minun sieluni asuisi hiljaisuuden maassa.
18 Niliposema, “Mguu wangu unateleza,” Ee Bwana, upendo wako ulinishikilia.
Kun minä ajattelen: "Minun jalkani horjuu", niin sinun armosi, Herra, minua tukee.
19 Wakati wasiwasi ulipokuwa mwingi ndani yangu, faraja yako ilinipa furaha nafsini mwangu.
Kun minulla on sydämessäni paljon murheita, niin sinun lohdutuksesi ilahuttaa minun sieluni.
20 Je, kiti cha utawala wa udhalimu kitajiunga nawe, ule utawala uletao taabu kutokana na sheria zake?
Onko yhteyttä sinun kanssasi turmion tuomioistuimella, jossa väkivaltaa tehdään lain varjolla,
21 Huungana kuwashambulia wenye haki, kuwahukumu kufa wasio na hatia.
ahdistetaan vanhurskaan sielua ja tuomitaan syylliseksi viaton veri?
22 Lakini Bwana amekuwa ngome yangu, na Mungu wangu amekuwa mwamba ninaoukimbilia.
Mutta Herra on minun linnani, Jumalani on minun suojakallioni.
23 Yeye atawalipa kwa ajili ya dhambi zao na atawaangamiza kwa ajili ya maovu yao; Bwana Mungu wetu atawaangamiza.
Hän kostaa heille heidän ilkityönsä ja hukuttaa heidät heidän pahuutensa tähden. Herra, meidän Jumalamme, hukuttaa heidät.