< Zaburi 91 >
1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
Los que viven bajo la protección del Altísimo, permanecerán seguros con el Todopoderoso.
2 Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
Esto es lo que diré del Señor: “Él es el único que me protege y me defiende. Él es mi Dios, y confío en él”.
3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
Porque él te salvará de trampas escondidas y de enfermedades mortales.
4 Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
Te esconderá bajo sus plumas, y te abrigará bajo sus alas. Su verdad te protegerá y te escudará.
5 Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
No tendrás miedo del terror nocturno, ni de las flechas que vuelan por el día,
6 wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
o de las enfermedades que atacan en la noche, o de catástrofes que caen al mediodía.
7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
Porque mil caerán a tu lado, y diez mil morirán a tu derecha, pero tú no serás dañado.
8 Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
Solo tendrás que abrir los ojos para que veas cómo los malos reciben su merecido.
9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
Ya que has hecho del Señor tu protección, y del Altísimo tu morada,
10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
nada malo te pasará; ninguna plaga se acercará donde vives.
11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
Porque él mandará a sus ángeles para que te cuiden en todo lo que hagas.
12 Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
Te sostendrán con sus manos para que no tropieces y caigas.
13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
Pisotearás leones y serpientes; hollarás crías de leones y víboras.
14 Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
Yo salvaré a todo el que me ame; protegeré a todo el que me acepte.
15 Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
Cuando clamen a mí pro ayuda, Responderé; cuando estén en problemas, Estaré con ellos. Los salvaré y los honraré.
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
Les daré una larga vida, y les mostraré mi salvación.