< Zaburi 91 >
1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
Живый в помощи Вышняго, в крове Бога небеснаго водворится,
2 Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
речет Господеви: заступник мой еси и прибежище мое, Бог мой, и уповаю на Него.
3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
Яко Той избавит тя от сети ловчи и от словесе мятежна:
4 Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
плещма Своима осенит тя, и под криле Его надеешися: оружием обыдет тя истина Его.
5 Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
Не убоишися от страха нощнаго, от стрелы летящия во дни,
6 wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
от вещи во тме преходящия, от сряща и беса полуденнаго.
7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
Падет от страны твоея тысяща, и тма одесную тебе, к тебе же не приближится:
8 Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
обаче очима твоима смотриши и воздаяние грешников узриши.
9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
Яко ты, Господи, упование мое: Вышняго положил еси прибежище твое.
10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
Не приидет к тебе зло, и рана не приближится телеси твоему:
11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
яко Ангелом Своим заповесть о тебе, сохранити тя во всех путех твоих.
12 Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
На руках возмут тя, да не когда преткнеши о камень ногу твою:
13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
на аспида и василиска наступиши, и попереши льва и змия.
14 Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
Яко на Мя упова, и избавлю и: покрыю и, яко позна имя Мое.
15 Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
Воззовет ко Мне, и услышу его: с ним есмь в скорби, изму его и прославлю его:
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
долготою дний исполню его и явлю ему спасение Мое.