< Zaburi 91 >

1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
Laus Cantici David. Qui habitat in adiutorio Altissimi, in protectione Dei caeli commorabitur.
2 Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
Dicet Domino: Susceptor meus es tu, et refugium meum: Deus meus sperabo in eum.
3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
Quoniam ipse liberavit me de laqueo venantium, et a verbo aspero.
4 Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
Scapulis suis obumbrabit tibi: et sub pennis eius sperabis:
5 Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
Scuto circumdabit te veritas eius: non timebis a timore nocturno,
6 wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
A sagitta volante in die, a negotio perambulante in tenebris: ab incursu, et daemonio meridiano.
7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
Cadent a latere tuo mille, et decem millia a dextris tuis: ad te autem non appropinquabit.
8 Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
Verumtamen oculis tuis considerabis: et retributionem peccatorum videbis.
9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
Quoniam tu es Domine spes mea: Altissimum posuisti refugium tuum.
10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
Non accedet ad te malum: et flagellum non appropinquabit tabernaculo tuo.
11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
Quoniam angelis suis mandavit de te: ut custodiant te in omnibus viis tuis.
12 Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
In manibus portabunt te: ne forte offendas ad lapidem pedem tuum.
13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
Super aspidem, et basiliscum ambulabis: et conculcabis leonem et draconem.
14 Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
Quoniam in me speravit, liberabo eum: protegam eum, quoniam cognovit nomen meum.
15 Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
Clamabit ad me, et ego exaudiam eum: cum ipso sum in tribulatione: eripiam eum et glorificabo eum.
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
Longitudine dierum replebo eum: et ostendam illi salutare meum.

< Zaburi 91 >