< Zaburi 91 >

1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
Celui qui habite dans la retraite du Très-Haut Repose à l'ombre du Tout-Puissant.
2 Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
Je dis à l'Éternel: «Tu es mon refuge et ma forteresse, Mon Dieu en qui je mets ma confiance!»
3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
C'est lui qui te délivrera du filet de l'oiseleur Et de la peste meurtrière.
4 Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
Il te couvrira de ses ailes. Et sous sa protection tu trouveras un refuge; Sa fidélité sera ton bouclier protecteur.
5 Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
Tu ne craindras ni les terreurs de la nuit. Ni la flèche qui vole pendant le jour,
6 wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
Ni la peste qui se glisse à travers les ténèbres, Ni la mortalité qui sévit en plein midi.
7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
Quand il tomberait mille hommes à ton côté Et dix mille à ta droite. Tu ne serais pas atteint.
8 Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
Mais toi, tu contempleras de tes yeux Et tu verras le châtiment des méchants.
9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
Oui, tu es mon refuge, ô Éternel! Tu as pris le Très-Haut pour ton asile.
10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
Aucun mal ne t'atteindra; Aucun fléau n'approchera de ta tente.
11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
Car il ordonnera à ses anges De te garder dans toutes tes entreprises.
12 Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
Ils te porteront sur leurs mains, De peur que ton pied ne heurte contre une pierre.
13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
Tu marcheras sur le lion et sur l'aspic; Tu écraseras le lionceau et le dragon.
14 Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
«Puisqu'il s'est attaché à moi, je le délivrerai; Je le mettrai en sûreté, puisqu'il connaît mon nom.
15 Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
Il m'invoquera, et je l'exaucerai; Je serai avec lui dans la détresse, Je l'en retirerai et je le glorifierai.
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
Je le rassasierai de longs jours. Et je lui ferai contempler mon salut.»

< Zaburi 91 >