< Zaburi 91 >
1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
Celui qui se tient dans la demeure du Souverain, se loge à l'ombre du Tout-Puissant.
2 Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
Je dirai à l'Eternel: Tu es ma retraite, et ma forteresse, tu es mon Dieu en qui je m'assure.
3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
Certes il te délivrera du filet du chasseur; [et] de la mortalité malheureuse.
4 Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
Il te couvrira de ses plumes, et tu auras retraite sous ses ailes; sa vérité [te servira de] rondache et de bouclier.
5 Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
Tu n'auras point peur de ce qui épouvante de nuit, ni de la flèche qui vole de jour.
6 wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
Ni de la mortalité qui marche dans les ténèbres; ni de la destruction qui fait le dégât en plein midi.
7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
Il en tombera mille à ton côté, et dix mille à ta droite; mais la [destruction] n'approchera point de toi.
8 Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
Seulement tu contempleras de tes yeux, et tu verras la récompense des méchants.
9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
Car tu es ma retraite, ô Eternel! tu as établi le Souverain pour ton domicile.
10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
Aucun mal ne te rencontrera, et aucune plaie n'approchera de ta tente.
11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
Car il donnera charge de toi à ses Anges, afin qu'ils te gardent en toutes tes voies.
12 Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
Ils te porteront dans leurs mains, de peur que ton pied ne heurte contre la pierre.
13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
Tu marcheras sur le lion et sur l'aspic, [et] tu fouleras le lionceau et le dragon.
14 Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
Puisqu'il m'aime avec affection, [dit le Seigneur], je le délivrerai; je le mettrai en une haute retraite, parce qu'il connaît mon Nom.
15 Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
Il m'invoquera, et je l'exaucerai; je serai avec lui dans la détresse, je l'en retirerai, et le glorifierai.
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
Je le rassasierai de jours, et je lui ferai voir ma délivrance.